1Sasa tuangalie mambo yale muliyoniandikia. Ni vizuri mwanaume asioe.
2Lakini kwa ajili ya kuepuka uasherati inafaa kila mwanaume akuwe na muke wake wa pekee, na kila mwanamuke akuwe na mume wake wa pekee.
3Mume anapaswa kumutimizia muke wake mapaswa yake, na muke anapaswa kumutimizia mume wake mapaswa yake.
4Muke hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa mume wake. Vilevile mume hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa muke wake.
5Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.
6Maneno hayo ninayowaambia si amri, lakini ni ruhusa tu ninayowapa.
7Hakika, ningetamani watu wote wakuwe kama mimi, lakini kila mutu amepewa zawadi yake ya kipekee na Mungu, mumoja zawadi hii, na mwingine zawadi ile.
8Na kwa wale wasiooa bado na wajane, ninawaambia kwamba ingekuwa vema waendelee kuishi peke yao kama vile mimi.
9Lakini kama hawawezi kujizuiza wao wenyewe, basi waoane; kwa maana afazali kuoa kuliko kuwaka tamaa.
10Kwa wale waliokwisha kuoana, ninatoa amri hii, isiyotoka kwangu, lakini kwa Bwana Mungu: muke hapaswi kuachana na mume wake.
11Lakini kama muke akiachana na mume wake, asiolewe tena, kama si vile apatane tena na mume wake. Vilevile mume hapaswi kufukuza muke wake.
12Na kwa wengine, mimi ninawaambia maneno haya, lakini hayatoki kwa Bwana: kama mume mwamini akiwa na muke asiyeamini, naye muke yule akikubali kuishi pamoja naye, asimufukuze.
13Vilevile kama muke mwamini akiwa na mume asiyeamini, naye mume yule akikubali kuishi pamoja naye, asiachane na mume wake.
14Kwa maana, mume asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na muke wake. Vilevile muke asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na mume wake. Kama isingekuwa vile, watoto wao wangehesabiwa kama watoto wa wapagani, lakini kwa hakika wao ni watu wa Mungu.
15Lakini kama mume au muke mupagani akitaka kuachana na mwamini aliyeoana naye, aachane naye. Katika mambo kama hayo, ndugu au dada mwamini yuko huru, kwa maana Mungu amewaita kusudi mukae katika amani.
16Wewe muke mwamini unaweza kujua namna gani kwamba utamwokoa mume wako? Au wewe mume mwamini utaweza kujua namna gani kwamba utamwokoa muke wako?
Kuishi kufuatana na mwito wa Mungu17Kwa ngambo ingine, kila mutu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote.
18Ikiwa mutu alitahiriwa mbele ya kuitwa na Mungu, asitafute kufuta kovu la kutahiriwa kwake. Ikiwa alikuwa hajatahiriwa wakati alipoitwa na Mungu, hapaswi kutahiriwa.
19Kutahiriwa au kutotahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni kutii amri za Mungu.
20Inafaa kila mutu abaki sawa alivyokuwa wakati alipoitwa na Mungu.
21Ikiwa ulikuwa mutumwa wakati Mungu alipokuita, usihuzunike. Lakini ikiwa kuna bahati ya kupata uhuru, usiipoteze bure.
22Kwa maana mutumwa aliyeitwa kuwa wa Bwana, amepewa uhuru na Bwana. Hivi vilevile mutu mwenye uhuru aliyeitwa na Kristo, ni mutumwa wa Kristo.
23Mumenunuliwa na Mungu kwa bei kali, basi musikuwe tena watumwa wa watu.
24Wandugu zangu, inafaa kila mutu akae katika ushirika wake na Mungu akibaki sawa alivyokuwa wakati alipoitwa naye.
Mafundisho juu ya mabikira na wajane25Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.
26Kwa sababu ya taabu ya siku hizi, ninafikiri kwamba ni vizuri mutu akae sawa vile anavyokuwa.
27Ikiwa umekwisha kuoa, usitafute kuachana na muke wako.
28Lakini kama ukioa, haufanyi zambi, na kama binti anaolewa, yeye hafanyi zambi vilevile. Lakini wale wanaooana watakuwa na mateso katika maisha yao, na mimi ninataka kuwaonya kusudi muepuke mateso yale.
29Wandugu zangu, mimi ninataka kusema hivi: wakati uliopangwa unabaki mufupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama vile wasiooa.
30Wale wanaolia wakuwe kama vile wasiolia. Wale wanaofurahi wakuwe kama vile wasiofurahi. Wale wanaonunua vitu wakuwe kama vile hawana kitu.
31Wale wanaotumia mali ya dunia hii wakuwe kama vile wasioitumia. Kwa maana dunia hii inakaribia kupita.
32Ningependa muishi bila masumbuko yoyote. Mutu asiyeoa anashugulikia mambo ya Bwana, anatafuta jinsi ya kumupendeza Bwana.
33Lakini mutu aliyeoa anasumbukia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kupendeza muke wake.
34Yeye anashugulikia mambo mawili. Vilevile mwanamuke asiyeolewa au binti anashugulikia mambo ya Bwana. Anajitolea kwa Bwana katika mawazo na matendo yake yote. Lakini mwanamuke anayeolewa, anashugulikia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kumupendeza mume wake.
35Maneno hayo ninayosema ni kwa faida yenu, wala si kwa kuwafungia njia. Ninataka kuwaonyesha namna ya kuishi sawa inavyofaa, kusudi mupate kumutumikia Bwana pasipo kizuizo chochote.
36Mutu akiona kwamba hamutendei muchumba wake vizuri, naye akitawaliwa na tamaa kwamba wangepaswa kuoana, basi afanye sawa vile anavyotaka. Yeye hafanyi zambi, waoane tu.
37Lakini inawezekana kwa mutu yule kuchunga kusudi lake bila kushurutishwa. Akiweza kutimiza sawa na mapenzi yake, akiamua kwamba hataki kumwoa muchumba wake, basi yeye anafanya vizuri kutomwoa.
38Hivi yule anayemwoa muchumba wake anafanya vizuri, na yule anayekataa kumwoa muchumba wake, anafanya vizuri zaidi.
39Mwanamuke aliyeolewa anafungwa na Sheria katika maisha yake na mume wake wakati mume wake angali muzima. Lakini kama mume wake akikufa, yeye ni huru kuolewa na yule anayetaka, lakini sherti ndoa ikuwe ya kikristo.
40Lakini ingekuwa heri zaidi kama angekaa sawa vile anavyokuwa. Hilo ni shauri langu, nami vilevile ninazani kwamba ninaongozwa na Roho wa Mungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.