1Ole wako muji wa mauaji!
Umejaa udanganyifu mutupu na wizi tele,
haukomi hata kidogo kunyanganya.
2Sikia! Mulio wa fimbo,
mashindo ya magurudumu,
vishindo vya farasi
na ngurumo za magari ya vita!
3Waaskari wapanda-farasi wanashambulia,
panga na mikuki inametameta;
waliouawa hawana hesabu,
kuna maiti nyingi sana;
watu wanajikwaa juu ya maiti!
4Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba.
Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi,
uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako,
na watu wa mataifa kwa uchawi wako.
5Mimi Yawe wa majeshi ninasema nitakushambulia;
nitapandisha nguo yako mpaka kwenye kichwa,
niyaache mataifa yauone uchi wako,
falme zitaona haya yako.
6Nitakutupia uchafu,
na kukuzaraulisha,
na kukufanya kuwa mushangao kwa watu.
7Kisha wote watakaokuona watakukimbia wakisema:
Ninawe umeangamizwa,
ni nani atakayekuomboleza?
Nani atakayekufariji?
8Wewe Ninawe, ni bora kuliko Tebe,
muji uliojengwa pembeni ya muto Nili?
Tebe ulizungukwa na maji,
bahari ilikuwa kikingio chake,
maji yalikuwa ukuta wake!
9Inchi ya Kushi ilikuwa nguvu yake;
nayo Misri vilevile, tena bila mwisho,
watu wa Puti na Libya waliusaidia.
10Hata hivyo, ulikamatwa mateka,
watu wake wakapelekwa katika uhamisho.
Hata watoto wake walipondwapondwa
katika maingilio ya kila barabara;
watu wake wenye heshima waligawanywa kwa kuwapigia kura,
wakubwa wake wote walifungwa minyororo.
11Ninawe, nawe vilevile utalewa;
utamukimbia adui na kujaribu kujificha.
12Kuta zako zote ni kama tini za kwanza;
zikitikiswa zinamwangukia mwenye kula katika kinywa.
13Angalia, waaskari wako ni wanawake tu.
Milango ya inchi yako ni wazi mbele ya waadui zako;
moto umeteketeza kabisa vifungio vyake.
14Muteke maji mukuwe tayari kwa kuzungukwa na vita;
muimarishe vikingio vyenu.
Muponde matope,
mutayarishe furu ya kuchomea matofali!
15Lakini kule vilevile moto utawateketeza,
upanga utawamaliza kabisa;
utawamaliza kama nzige wanavyokula.
Muongezeke kama nzige,
mwongezeke kama mapanzi!
16Wachuuzi wako waliongezeka kuliko nyota;
lakini sasa wametoweka kama vile mapanzi wanavyoruka.
17Wakubwa wako ni kama mapanzi,
majemadari wako kama kundi la nzige;
wakati wa baridi wanakaa kwenye kuta,
lakini jua linapotokea, wanaruka,
wala hakuna anayejua nafasi walipokwenda.
18Ewe mufalme wa Asuria, wachungaji wako wamelala,
waheshimiwa wako wamesinzia.
Watu wako wametawanyika kwenye milima,
wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.
19Hakuna wa kutunza mapigo yako,
vidonda vyako ni vya kifo.
Wote wanaosikia habari zako wanashangilia.
Maana ni nani aliyeponyoka kila mara uovu wako?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.