1Siku hiyo, Debora na Baraka mwana wa Abinoamu, wakaimba wimbo huu:
2Viongozi walijitokeza kuongoza Israeli,
watu walijitolea kwa mapenzi yao.
Mumushukuru Yawe!
3Musikilize, enyi wafalme!
Mutege sikio, enyi wakubwa!
Nitamwimbia Yawe, Mungu wa Israeli.
4Ee Yawe,
ulipotoka kule Seiri,
ulipoteremuka kwenye mulima Edomu,
inchi ilitetemeka,
mbingu zilidondosha maji,
mawingu yakaiangusha mvua.
5Milima ilitikisika mbele yako Yawe,
mulima Sinai mbele yako Yawe,
Mungu wa Israeli.
6Katika siku za Samugari mwana wa Anati,
katika wakati wa Yaeli,
makundi ya watu yalikoma kupita katika inchi,
wasafiri walipitia njia za pembenipembeni.
7Walimaji walitoweka,
walitoweka katika Israeli,
mpaka nilipotokea mimi Debora,
mimi ninayekuwa mama wa Israeli.
8Walijichagulia miungu mipya,
kukakuwa vita katika inchi.
Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngao
kati ya watu elfu makumi ine wa Israeli.
9Ninawapa heshima viongozi wa Israeli
waliojitoa kwa mapenzi yao kati ya watu.
Mushukuru Yawe!
10Enyi munaopanda juu ya punda weupe,
enyi munaoikalia matandiko ya bei kali,
enyi munaotembea katika njia,
mutangaze jambo hilo!
11Kwenye visima vya maji,
tangaza ushindi wa Yawe,
ushindi kwa walimaji wake katika Israeli.
Watu wa Yawe walishuka kwenye mulango wa muji.
12“Amuka, amuka, Debora!
Amuka! Amuka uimbe wimbo!
Amuka, Baraka mwana wa Abinoamu,
uwakamate wafungwa wako.
13Mashujaa waliobaki waliteremuka.
Watu wa Yawe walikwenda
kumupigania na wenye nguvu.
14Kutoka Efuraimu waliteremuka katika bonde,
wakafuata wandugu zao watu wa Benjamina;
kutoka Makiri, majemadari walishuka,
kutoka Zebuluni, wenye fimbo ya mutawala.
15Wakubwa wa Isakari wakafuata Debora,
watu wa Isakari, waaminifu kwa Baraka,
wakamufuata mbio mpaka katika bonde.
Lakini kati ya ukoo za Rubeni
kulikuwa kusitasita kwingi.
16Kwa nini walibaki katika mazizi?
Kwa kusikiliza milio ya kondoo?
Kati ya ukoo za Rubeni
kulikuwa kusitasita kwingi.
17Kabila la Gileadi lilibaki ngambo ya Yordani.
Kabila la Dani, kwa nini mulibaki ndani ya mashua?
Kabila la Aseri lilitulia kule pembeni ya bahari,
lilikaa katika kivuko chake.
18Watu wa Zebuluni ni watu
waliohatarisha maisha yao katika kifo.
Hata wa Nafutali walisogelea kifo
kwenye miinuko ya mashamba.
19“Kule Tanaki, pembeni ya chemichemi za Megido,
wafalme walikuja, wakapigana;
wafalme wa Kanana walipigana,
lakini hawakuteka feza.
20Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita,
zilifuata njia zao zikapigana na Sisera.
21Mafuriko ya muto Kisoni yaliwapeleka mbali,
mafuriko makali ya muto Kisoni.
Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!
22“Farasi walipita wakipiga udongo,
walipigapiga udongo na kishindo cha kwato zao.
23Malaika wa Yawe anasema hivi:
‘Ulaani muji wa Merosi,
uwalaani vikali wakaaji wake;
maana hawakukuja kumusaidia Yawe
hawakumusaidia Yawe juu ya wenye nguvu’.
24“Abarikiwe kuliko wanawake wote
Yaeli, muke wa Heberi Mukeni.
Amebarikiwa kuliko wanawake wote
wanaokaa katika mahema.
25Sisera alimwomba maji,
naye akamupa maziwa;
akamuletea siagi
katika bakuli ya heshima.
26Kwa mukono mumoja
akashika musumari wa kufungia hema,
na kwa mukono wake wa kuume
nyundo ya fundi.
Alimuponda Sisera kichwa,
akavunja na kupasuapasua paji lake.
27Sisera akainama, akaanguka;
akalala kimya kwenye miguu yake.
Hapo alipoinama ndipo alipoanguka amekufa!
28“Mama ya Sisera
akaangalia toka kwenye dirisha,
akachungulia, kisha akalalamika:
‘Kwa nini gari lake limechelewa?
Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa kusikilika?’
29Jibu akalipata kwa wanawake wenye hekima:
akajituliza tena na tena kwa jibu hilo:
30‘Bila shaka wanatafuta na kugawanyana vitu:
binti mumoja au wawili kwa kila askari,
nguo ya sufu ya rangi kwa ajili ya Sisera,
nguo ya sufu iliyopindwa vizuri,
na mikufu miwili yenye kufumwa kwa ajili ya shingo yangu!’
31“Ee Yawe,
waangamie waadui zako wote!
Lakini warafiki zako wakuwe kama jua,
wakati linapochomoza kwa mwangaza mukubwa!”
Inchi ya Waisraeli ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi ine.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.