1Tulipokwisha kuponyoka kufa, ndio wakati tulijua kwamba kisanga kile tulichokuwa ndani yake kinaitwa Melita.
2Wenyeji wa kule wakatutendea mema sana. Mvua ilikuwa imeanza kunyesha na kulikuwa baridi, kwa hiyo watu wale wakatukongea moto na kutukaribisha sisi wote.
3Paulo akatwaa lundo ya kuni, na alipokuwa akiiweka ndani ya moto, nyoka akatoka katikati ya ile lundo kwa sababu ya kivukuto na kujizingia kwa mukono wake.
4Wale wenyeji wa kule walipoona nyoka yule anajizingia kwa mukono wake wakasemezana: “Hakika mutu huyu ni mwuaji, kwa maana ijapokuwa alipona katika hatari ya bahari, kufuatana na azabu ya haki ya Mungu, kufa kwake kunatimia.”
5Lakini Paulo akamukungutia yule nyoka katika moto wala hakumuzuru hata kidogo.
6Nao watu wale walingojea kuona ikiwa atavimba mukono au ataanguka mara moja na kufa. Lakini kisha kungoja muda murefu na kuona kwamba hakupata hasara yoyote, wakabadilisha mawazo yao hata wakasema kwamba yeye ni mumoja wa miungu.
7Karibu na pale kulikuwa mashamba ya mukubwa wa kisanga, aliyeitwa Publio. Mutu yule akatukaribisha kwa upendo na kutupangisha ndani ya nyumba yake kwa muda wa siku tatu.
8Baba ya Publio alikuwa amelala kwa ajili ya kuwezwa na ugonjwa wa homa na wa kuhara damu. Paulo akaenda kumwangalia, akamwombea na kuweka mikono juu yake, naye akapona.
9Na kufuatana na jambo hilo, wagonjwa wengine waliokaa katika kisanga kile wakakuja, nao wakaponyeshwa vilevile.
10Watu wakatuheshimu sana, na wakati tulipoondoka kwa njia ya chombo kwa kuendelea wakatupatia vitu vyote tulivyohitaji kwa safari yetu.
Paulo na wenzake wanafika Roma11Kulipopita miezi mitatu, tukasafiri katika chombo kimoja kilichobaki katika kisanga kile kwa kungojea wakati wa baridi kali upite kwanza. Chombo kile kilikuwa chenye kutoka Alesanduria. Na juu yake kulikuwa michoro ya sanamu za mapacha ya miungu.
12Tulipofika Sirakuse, tukakaa kule kwa muda wa siku tatu.
13Kutoka kule tukazunguka pembenipembeni ya bahari hata tukafika katika muji Regio. Kesho yake upepo usiokuwa mukali ukaanza kuvuma tokea kusini, na kwa mwendo wa siku mbili tukafika katika muji Puteoli.
14Kule tukakuta wandugu waamini, nao wakatualika tukae pamoja nao kwa muda wa juma moja. Ni vile tulivyosafiri hata kufika Roma.
15Wandugu waamini wa Roma waliposikia habari zetu wakakuja kutuona kwenye Soko la Apio na wengine kwenye Tiretaberne. Paulo alipowaona, akamushukuru Mungu na kutiwa tena moyo.
16Tulipofika Roma, Paulo akapewa ruhusa ya kujilipia nyumba ya kupanga ambamo atakaa pamoja na askari mumoja mwenye kumuchunga.
Paulo anahubiri katika Roma17Kulipopita siku tatu, Paulo aliwaita wakubwa wa Wayuda waliokaa kule. Na walipokwisha kukusanyika akawaambia: “Wandugu, mimi nilifungwa kule Yerusalema na kutolewa kwa Waroma ijapokuwa sikufanya kosa lolote juu ya taifa letu wala kuvunja desturi za babu zetu.
18Nao walipokwisha kunisambisha, walitaka kunifungua kwa sababu hawakuniona na kosa linalonipasa kuuawa.
19Lakini nilipoona kwamba Wayuda wanakataa shauri lile, ilinilazimisha kuomba nisambishwe na Mufalme wa Roma. Na katika haya yote sikukuwa na mashitaki yoyote juu ya taifa langu.
20Basi ni kwa sababu hii nimewaita kusudi tuonane na niseme nanyi, kwa maana ninafungwa na munyororo huu kwa ajili ya tumaini ambalo Waisraeli wanakuwa nalo.”
21Wakamwambia: “Sisi hatukupokea barua juu yako toka Yudea, wala ndugu Muyuda aliyefika huku kwa kutupasha habari, wala kusema ubaya juu yako.
22Lakini tungependa kusikia mawazo yako kwa maana tunajua kwamba fasi zote watu wanapinga dini hii unayofuata.”
23Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.
24Wamoja wakasadiki maneno yaliyosemwa, lakini wengine hawakuyaamini.
25Nao walipokuwa wakiondoka bila kupatana, Paulo akaongeza kuwaambia maneno haya tu: “Roho Mutakatifu alikuwa na sheria ya kusema hivi kwa babu zenu kwa njia ya nabii Isaya:
26Uwaendee watu hawa na kuwaambia:
Kusikia mutasikia, lakini hamutafahamu.
Kuangalia mutaangalia, lakini hamutatambua.
27Maana mioyo ya watu hawa imegeuka kuwa migumu,
wameziba masikio yao na
wamefunga macho yao.
Isingekuwa hivi,
wangeona na macho yao, wangesikia na masikio yao,
wangefahamu na mioyo yao, na wangegeukia kwangu na ningewaponyesha.
28“Na kwa kumaliza, basi mujue kwamba habari ya wokovu huu wa Mungu imetumwa kutangazwa kwa watu wa mataifa mengine, nao wataisikia!”
[
29Paulo alipokwisha kusema maneno haya, Wayuda wakaenda wakibishana sana wao kwa wao.]
30Paulo akakaa miaka miwili katika nyumba aliyokuwa akijilipia yeye mwenyewe. Alikaribisha watu wote waliokuja kumwona.
31Alihubiri habari za Ufalme wa Mungu na kuwafundisha watu juu ya Bwana Yesu Kristo bila woga na bila kuzuizwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.