1Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.
2Matendo yote ya mutu ni sawa katika macho yake, lakini Yawe anapima mioyo.
3Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.
4Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.
5Mipango ya mutu wa bidii inaleta mali kwa wingi, lakini kila mutu anayetenda kwa harakaharaka anapata umasikini.
6Mali inayopatikana kwa udanganyifu ni muvuke unaopita na mutego wa kifo.
7Ukali wa waovu utawaangamiza, maana wanakataa kutenda mambo ya haki.
8Njia ya mutu mwenye kosa imepotoka, lakini mwenendo wa mwenye moyo safi ni sawa.
9Afazali kuishi pembeni juu ya paa, kuliko kuishi ndani ya nyumba pamoja na mwanamuke mugomvi.
10Mutu mwovu anatamani kutenda uovu; hata kwa jirani yake hana huruma.
11Mwenye kiburi anapoazibiwa, mujinga anapata hekima. Ukimufundisha mwenye hekima, unamupatia maarifa.
12Mwenye haki anajua yanayokuwa katika nyumba ya waovu: waovu wanaangushwa chini na kuangamia.
13Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.
14Hasira inatulizwa kwa zawadi ya siri; kituliro kinachotolewa kwa uficho kinatuliza kasirani.
15Haki ya sheria ikifuatwa, watu wema wanafurahi lakini watu waovu wanafazaika.
16Anayetangatanga mbali na njia ya ufahamu, atajikuta ametua kati ya wafu.
17Anayependa raha atakuwa masikini; anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.
18Mwovu atakuwa malipo kwa ukombozi wa wenye haki; nao wasiokuwa waaminifu kwa pahali pa watu wa usawa.
19Afazali kuishi katika jangwa kuliko kukaa na mwanamuke mugomvi na muchokozi.
20Katika nyumba ya mwenye hekima kuna hazina za bei kali, lakini mupumbafu anaponda mali yake yote.
21Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.
22Mwenye hekima anaweza kuteka muji wa wenye nguvu na kukiporomosha kikingio wanachokitegemea.
23Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.
24Mwenye kiburi na majivuno jina lake ni “Mazarau”; anatenda kwa kujivuna tu.
25Muvivu anakufa kwa kutokutimizwa kwa tamaa zake, maana mikono yake haitaki kufanya kazi.
26Muchana kutwa mwovu anatamani kupata kitu, lakini mwenye haki anatoa, tena bila mipaka.
27Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.
28Mushuhuda mwongo ataangamia, lakini anayejua kusikiliza hawezi kunyamazishwa.
29Mutu mwovu anajionyesha kuwa hodari, lakini mutu wa usawa anafikiri vizuri juu ya mwenendo wake.
30Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.
31Farasi anatayarishwa kwa vita, lakini ushindi unaletwa na Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.