1Hawa ndio wazao wa Haruni na Musa wakati Yawe alipozungumuza na Musa kwenye mulima Sinai.
2Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni: Nadabu, muzaliwa wake wa kwanza, Abihu, Eleazari na Itamari. Walawi wanachaguliwa kwa kutumikia makuhani
5Yawe akamwambia Musa:
6Uwalete karibu watu wa kabila la Lawi, uwaweke mbele ya kuhani Haruni wapate kumutumikia.
7Watafanya kazi kwa pahali pake na pa Waisraeli wote pamoja kwenye hema la mukutano wanapotumika pale.
8Watatunza vyombo vyote vya hema la mukutano na kuwasaidia Waisraeli wanapofanya kazi zao kwenye hema takatifu.
9Utamupatia Haruni Walawi na wazao wake makuhani; hao wametolewa kwake kabisa kati ya Waisraeli.
10Utachagua Haruni na wana wake kusudi waweze kutimiza kazi zao za ukuhani; lakini kama mutu yeyote mwingine akikaribia, atauawa.
11Yawe akaendelea kumwambia Musa:
12Sasa nimechagua Walawi kati ya Waisraeli wote, pahali pa kila muzaliwa wa kwanza mwanaume anayefungua tumbo la mama yake katika kila jamaa ya Israeli. Walawi ni wangu,
13maana kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu hata wa nyama; wao watakuwa wangu. Mimi ni Yawe. Kuhesabiwa kwa Walawi
14Yawe akamwambia Musa katika jangwa la Sinai:
15Uwahesabu wana wa Walawi wote kulingana na ukoo zao na jamaa zao, kila mwanaume kuanzia watoto wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi.
16Basi, Musa akawahesabu kufuatana na neno la Yawe, kama vile alivyomwamuru.
17Hawa ndio waliokuwa wana wa Lawi: Gersoni, Kohati na Merari.
18Na haya ndiyo majina ya wana wa Gersoni kwa kufuata jamaa zao: Libuni na Simei.
19Wana wa Kohati kwa kufuata jamaa zao: Amuramu, Isihari, Hebroni na Uzieli.
20Wana wa Merari kwa kufuata jamaa zao: Mali na Musi. Hizi zilikuwa jamaa za Walawi kulingana na ukoo zao.
21Jamaa za Walibuni na Wasimei zilitokana na Gersoni; hizi ndizo zilizokuwa jamaa za Wagersoni.
22Hesabu yao kwa kadiri ya hesabu ya wanaume wote kuanzia waliokuwa na mwezi mumoja na zaidi ni elfu saba na mia tano.
23Ilipasa kwa jamaa za Wagersoni kupiga kambi yao upande wa magaribi, nyuma ya hema takatifu
24naye Eliasafu mwana wa Laeli akiwa mukubwa wa ukoo wa Wagersoni.
25Kazi ya wana wa Gersoni ilikuwa kutunza hema takatifu, hema pamoja na kifuniko chake, pazia la mulango wa hema la mukutano,
26mapazia ya upango unaokuwa kati ya hema takatifu na mazabahu, na pazia la mulango wa upango, na kamba zake. Kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa zao.
27Jamaa za Waamuramu, Waisari, Wahebroni na Wauzieli zilitokana na Kohati; hizi ndizo zilizokuwa jamaa za Wakohati.
28Kadiri ya hesabu ya wanaume wote kuanzia wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu nane na mia sita, waliotumika katika Pahali Patakatifu.
29Jamaa za wana wa Kohati watapiga kambi yao upande wa kusini wa hema takatifu,
30naye Elisafani, akiwa mukubwa wa ukoo huo wa jamaa za Wakohati.
31Wao walioshugulika na kazi ya kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, mazabahu, vyombo makuhani wanavyotumia hema takatifu na pazia; kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa zao.
32Naye Eleazari mwana wa kuhani Haruni aliwekwa kuwa mukubwa wa wakubwa wa Walawi, na musimamizi wa watumishi wote wa Pahali Patakatifu.
33Jamaa za Wamali na Wamusi zilitokana na Merari;
34hizi ndizo jamaa za Merari. Hesabu yao kadiri ya hesabu ya wanaume wote kuanzia wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa watu elfu sita na mia mbili.
35Mukubwa wa ukoo wa jamaa za Merari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa watapiga kambi yao upande wa kaskazini wa hema takatifu.
36Wao walipewa kazi ya kutunza mbao za hema takatifu, miti yake, nguzo, vitako na vifaa vyote vya kushikilia hema; kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa juu yao.
37Vielvile walihitajika kutunza nguzo za upango zilizouzunguka na vitako vyake, misumari na kamba zake.
38Musa na Haruni na wana wao watapiga kambi yao mbele ya hema takatifu upande wa mashariki, ni kusema mbele ya hema la mukutano kuelekea upande linakotokea jua. Kazi yao itakuwa kutumika kwenye Pahali Patakatifu kwa jambo lolote lililohitajika kufanyika kwa ajili ya Waisraeli. Mutu mwingine yeyote aliyesogea karibu alipaswa kuuawa.
39Hesabu ya Walawi kulingana na jamaa zao, wanaume wote kuanzia watoto wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ambao Musa na Haruni waliwahesabu kwa amri ya Yawe, ilikuwa watu elfu makumi mbili na mbili.
Walawi pahali pa wazaliwa wa kwanza40Kisha Yawe akamwambia Musa: Uwahesabu kwa majina wazaliwa wa kwanza wanaume wote wa Waisraeli kuanzia wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi.
41Nawe utatenga Walawi kwa ajili yangu mimi Yawe; vilevile utatenga kwa ajili yangu mifugo yote ya Walawi pahali pa wazaliwa wa kwanza wa ngombe za watu wa Israeli.
42Basi, Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa watu wa Israeli kama vile Yawe alivyomwamuru.
43Wote wazaliwa wa kwanza wanaume kadiri ya hesabu ya majina, kuanzia wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi, kufuata jinsi walivyohesabiwa, walikuwa elfu makumi mbili na mbili mia mbili makumi saba na tatu.
44Yawe akamwambia Musa:
45Sasa, utenge Walawi wote kuwa wangu pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli. Vilevile, utenge ngombe wa Walawi wote pahali pa wazaliwa wa kwanza wa ngombe wa Waisraeli. Mimi ni Yawe.
46Kwa ajili ya malipo ya wazaliwa wa kwanza wanaume wa watu wa Israeli mia mbili makumi saba na watatu, wanaozidi hesabu ya wanaume Walawi,
47utapokea kwa kila mwanaume feza shekeli tano, kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu, ambayo ni sawa na gera makumi mbili,
48na feza hizo kwa ajili ya malipo ya hao waliozidi hesabu yao utamupa Haruni na wana wake.
49Musa akatii, akatwaa feza hizo za malipo ya hao waliozidi hesabu ya waliolipiwa na Walawi;
50akapokea kutoka wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli feza kiasi cha shekeli elfu moja mia tatu makumi sita na tano, kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu,
51akawapa Haruni na wana wake feza hizo za malipo sawa na neno la Yawe, kama vile alivyomwamuru.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.