Ezekieli 25 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Unabii juu ya Waamoni

1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Ang. Yer 49.1-5; Eze 21.28-30; Amo 1.13-15; Zef 2.8-11

2Wewe mwanadamu! Ugeukie upande wa inchi ya Waamoni, utoe unabii juu yao.

3Uwaambie Waamoni hivi: Musikilize neno la Bwana wetu Yawe: Ninyi mulifurahia kuona hekalu langu likichafuliwa, inchi ya Waisraeli ikiangamizwa na watu wa Yuda wakipelekwa katika uhamisho.

4Basi, nitawatoa ninyi katika mikono ya watu wa mashariki; watapiga hema zao kati yenu na kufanya makao yao katika inchi yenu. Nao watakula matunda yenu na kunywa maziwa yenu.

5Nitaufanya muji wa Raba kuwa nafasi ya kukulishia ngamia na inchi ya Amoni kuwa zizi la kondoo. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.

6Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu mulipiga mikono, mukarukaruka kwa furaha na kushangilia sana juu ya inchi ya Waisraeli,

7basi, mimi nimeunyoosha mukono juu yenu kwa kuwaazibu; nitawaacha mukamatwe mateka na watu wa mataifa mengine. Nitawaangamiza kabisa, nanyi hamutakuwa taifa tena wala kuwa na inchi. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.

Unabii juu ya Moabu

8Bwana wetu Yawe alisema: Kwa sababu Wamoabu wamesema kwamba watu wa inchi ya Yuda ni sawa tu na mataifa mengine, Ang. Isa 15.1–16.14; 25.10-12; Yer 48.1-47; Amo 2.1-3; Zef 2.8-11

9mimi nitaifanya miji inayolinda mipaka ya Moabu ishambuliwe, hata miji ile bora kabisa, ni kusema Beti-Yesimoti, Bali-Meoni na Kiriataimu.

10Nitatoa inchi hiyo pamoja na inchi ya Waamoni katika mikono ya watu wa mashariki wakuwe mali yao. Inchi ya Moabu haitakuwa taifa tena.

11Mimi nitaiazibu inchi ya Moabu, nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.

Unabii juu ya Waedomu

12Bwana wetu Yawe alisema hivi: Kwa sababu Waedomu wamefanya kisasi na Yuda, wakawalipiza watu wa Yuda kisasi kibaya sana Ang. Isa 34.5-17; 63.1-6; Yer 49.7-22; Eze 35.1-15; Amo 1.11-12; Oba 1-14; Mal 1.2-5

13basi, Bwana wetu Yawe anasema: Nitanyoosha mukono juu ya inchi ya Edomu kwa kuwaazibu na kuwaua watu wote na nyama. Nitaifanya kuwa ukiwa kutoka muji wa Temani mpaka muji wa Dedani. Watu wa inchi hiyo watauawa kwa upanga.

14Nitawafanya watu wangu Waisraeli walipize kisasi juu ya Waedomu nao watawatendea Waedomu kadiri ya hasira na kasirani yangu. Halafu Waedomu watatambua uzito wa kisasi changu.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

Unabii juu ya Wafilistini

15Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu Wafilistini walifanya kisasi, wakawalipiza kisasi waadui zao kwa ubaya sana na kuendelea kuwa waadui zao siku zote, Ang. Isa 14.29-31; Yer 47.1-7; Yoe 3.4-8; Amo 1.6-8; Zef 2.4-7; Zak 9.5-7

16basi, mimi Bwana wenu Yawe ninawaambia hivi:

Nitanyoosha mukono juu ya Wafilistini kwa kuwaazibu; nitawaangamiza hao watu wa Kereti na wakaaji wa kandokando ya bahari.

17Nitawalipiza kisasi kikali kwa azabu ya kasirani. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help