Ezekieli 44 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Matumizi ya mulango wa mashariki

1Yule mutu akanirudisha kwenye mulango wa inje unaoelekea upande wa mashariki, inje ya pahali patakatifu, nao ulikuwa umefungwa.

2Yawe akaniambia hivi: Mulango huu utaendelea kufungwa. Hakuna mutu yeyote anayeruhusiwa kuutumia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wa Israeli, nimeingia kupitia mulango ule. Hivyo utadumu ukiwa umefungwa.

3Hata hivyo, mukubwa anayetawala anaweza kwenda huko na kula chakula chake kitakatifu mbele yangu. Anapaswa kuingia na kutokea kwenye mulango wa chumba cha kuingilia.

Kawaida za kuingia katika hekalu

4Yule mutu akanipeleka mbele ya nyumba ya Yawe, kwa njia ya mulango wa kaskazini. Nilipoangalia, nikaona utukufu wa Yawe umeijaza nyumba ya Yawe. Hapo nikaanguka uso mpaka chini.

5Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Angalia vizuri mambo yote unayoona na kusikia. Nitakuelezea maagizo yote ya nyumba ya Yawe na sheria zake zote. Shika ndani ya moyo wako kwa uangalifu, ni watu gani wanaoruhusiwa kuingia na kutoka katika nyumba ya Yawe na ni watu gani wamekatazwa kuingia humo.

6Utawaambia hao watu waasi wa Israeli hivi:

Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siwezi kuendelea kuyavumilia machukizo yenu yote.

7Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.

8Kisha kutimiza kazi ya vitu vyangu vitakatifu, mumeruhusu watu wa mataifa mengine kutimiza kazi hiyo katika hekalu langu.

9Sasa, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Hakuna mutu yeyote wa taifa la kigeni, asiyetahiriwa au asiyenitii mimi atakayeruhusiwa kuingia katika hekalu langu; hata wageni wanaoishi kati ya Waisraeli, hawataruhusiwa.

Walawi wanaondolewa kwenye ukuhani

10Walawi walioniacha wakati ule Waisraeli walipojitenga nami kwa kufuata miungu yao, watabeba azabu yao.

11Wataweza tu kutumika katika hekalu langu kama watumishi wakilinda milango ya nyumba yangu, na kutumikia katika nyumba. Wataweza kuchinja nyama wanaotolewa na watu kwa ajili ya kutolewa sadaka za kuteketeza na kuwatumikia watu.

12Lakini kwa sababu waliongoza ibada za miungu kwa ajili ya watu wa Israeli, wakasukuma watu kutenda zambi, basi, nimeunyoosha mukono wangu kuwaazibu.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–

Nao watabeba azabu yao.

13Hawatakaribia mbele yangu tena kwa kunitumikia kama makuhani, wala hawatavigusa tena vitu vitakatifu wala vile vitakatifu sana. Lakini watapata haya kwa sababu ya machukizo yao waliyotenda.

14Hata hivyo, watashika zamu ya kulinda nyumba, wakifanya kazi yote na kazi zote zitakazotendeka humo.

Makuhani

15Lakini makuhani wa kabila la Lawi ambao ni wazao wa Zadoki walioendelesha kazi yangu katika pahali patakatifu pangu, wakati Waisraeli waliponiacha, hao ndio watakaoendelea kunitumikia na kuja mbele yangu kunitolea mafuta na damu.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–

16Hao tu ndio watakaoingia katika hekalu langu, nao watakaribia kwenye mazabahu kwa kunitumikia.

17Lakini wanapoingia katika kiwanja cha ndani, watavaa nguo za kitani; hawatavaa nguo za sufu watakapotumika katika milango ya kiwanja cha ndani na kwenye nyumba. Ang. Kut 28.39-43; Law 16.4

18Watavaa vitambaa vya kitani kwenye vichwa vyao, na makapitula za kitani katika viuno vyao; lakini bila mukaba wowote kwa kuepuka jasho.

19Watakapotoka kwenda kwenye kiwanja cha inje kwa watu, watatosha nguo walizovaa wakati walipokuwa wanatumika na kuziweka katika vyumba vitakatifu. Ni lazima wavae nguo zingine, kusudi watu wasijitakase kwa kugusa nguo zao.

20Hawatanyoa vichwa vyao wala kuacha nywele zao zikuwe ndefu. Lakini watapunguza nywele zao.

21Kuhani yeyote asikunywe divai anapoingia katika kiwanja cha ndani.

22Kuhani yeyote asioe mwanamuke mujane wala mwanamuke aliyeachana na mume wake. Lakini atamwoa bikira ambaye ni Mwisraeli au mwanamuke aliyefiwa na mume wake aliyekuwa kuhani.

23Makuhani watafundisha taifa langu kupambanua vitu vinavyokuwa vitakatifu na visivyokuwa vitakatifu, na kuwajulisha tofauti kati ya vitu vinavyokuwa vichafu na visivyokuwa vichafu.

24Kukikuwa magombano wataamua kadiri ya maamuzi yangu. Katika sikukuu zote watafuata sheria zangu na maamuzi yangu, na kuzitakasa Sabato zangu.

25Hawatasogelea maiti kusudi wasijichafue. Lakini wataweza kujichafua kwa kusogelea maiti ya baba au mama au mutoto wa kike au wa kiume au dada asiyeolewa.

26Mumoja wao akijichafua, atakaa na hali hiyo kwa muda wa siku saba. Kisha atakuwa safi.

27Siku atakapoingia katika patakatifu, katika kiwanja cha ndani kwa kutumika, atatoa sadaka yake ya kusamehewa zambi.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

28Makuhani hawatakuwa na haki ya kurizi inchi; haki yao ni kunitumikia mimi. Hamutawapa urizi katika inchi ya Israeli, watakachokuwa nacho ni mimi tu.

29Watakula sadaka ya vyakula, sadaka ya kusamehewa zambi, na sadaka ya malipo ya kosa. Kila kitu katika Israeli kilichotakaswa kwa Mungu kitakuwa chao. Ang. Hes 18.8-19

30Sehemu ya kwanza ya malimbuko yenu na vya matoleo yenu ya kila aina vitakuwa kwa ajili ya makuhani. Tena mutawapa sehemu ya kwanza ya unga wenu, kusudi mulete baraka juu ya nyumba zenu.

31Makuhani hawatakula nyamafu au ndege yeyote aliyekufa mwenyewe au aliyeraruliwa na nyama wa pori.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help