1Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala Yuda, akatawala kutoka Yerusalema kwa muda wa miaka makumi tano na mitano.
2Alitenda maovu mbele ya Yawe kwa kutenda maovu ya mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe mbele ya watu wa Israeli.
3Alitengeneza upya nafasi za kuabudia miungu mingine zilizoharibiwa na baba yake Hezekia. Akajenga mazabahu za kuabudia Bali na kutengeneza sanamu ya Ashera, kama vile Ahabu mufalme wa Israeli alivyofanya. Vilevile, Manase aliabudu na kutumikia jeshi la mbingu.
4Alijenga mazabahu katika nyumba ya Yawe pahali ambapo Yawe alikuwa amesema: “Jina langu litaabudiwa katika Yerusalema.”
5Katika viwanja viwili vya nyumba ya Yawe, alijenga mazabahu ya kuabudia jeshi la mbingu.
6Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.
7Nayo sanamu ya Ashera aliyotengeneza akaiweka katika nyumba ambayo Yawe alisema juu yake mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema niliouchagua ndipo pahali nitakapoabudiwa milele.
8Na ikiwa Waisraeli watajali kutenda yote niliyowaamuru na kufuata sheria zote mutumishi wangu Musa alizowapa, basi sitawaacha wafukuzwe kutoka katika inchi hii ambayo niliwapa babu zao.”
9Lakini hawakusikia, naye Manase aliwasukuma watende zambi zaidi kuliko zile zilizofanywa na mataifa ambayo Yawe aliyaharibu mbele ya Waisraeli.
10Halafu Yawe akasema kupitia kwa watumishi wake manabii:
11“Kwa sababu mufalme amefanya mambo ya kuchukiza, mambo mabaya zaidi ya yale yaliyotendwa na Waamori waliomutangulia, akawasukuma watu wa Yuda vilevile watende zambi kwa kutumia sanamu zake,
12basi, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitaleta juu ya Yerusalema na Yuda hasara ambayo hata yeyote atakayesikia atashituka.
13Nitauazibu Yerusalema kama vile nilivyofanya Samaria, na mufalme Ahabu na wazao wake. Nitasafisha Yerusalema kama vile wanavyosafisha sahani na kuigeuza kisha kusafishwa.
14Nitawaacha hao watu wa urizi wangu watakaobaki na kuwaweka katika mikono ya waadui zao, watanyanganywa vitu vyao na kutekwa na waadui zao wote.
15Nitawatendea hayo yote kwa sababu wameniasi na kunikasirikisha tangia wakati wazee wao walipotoka Misri mpaka leo.”
16Zaidi ya mambo hayo, Manase aliwaangusha watu wa Yuda katika zambi kwa kutenda maovu mbele ya Yawe. Aliwaua watu wengi wasiokuwa na kosa, damu ikajaa toka upande mumoja mpaka upande mwingine wa Yerusalema.
17Mambo mengine ya Manase na yote aliyofanya, pamoja na zambi zake zote, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
18Manase akakufa na kuzikwa katika bustani ya nyumba yake mwenyewe, katika Bustani ya Uza. Naye mwana wake Amoni akatawala kwa pahali pake.
Mufalme Amoni wa Yuda(2 Sik 33.21-25)19Amoni alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mbili alipoanza kutawala, akatawala miaka miwili akiwa kule Yerusalema. Jina la mama yake ni Mesulemeti binti ya Haruzi, wa muji Yotibati.
20Alitenda maovu mbele ya Yawe, kama vile Manase baba yake alivyofanya.
21Alifuata njia yote baba yake aliyoiendea na kutumikia sanamu ambazo baba yake alizitumikia na kuziabudu.
22Alimwacha Yawe, Mungu wa babu zake. Hakushika njia ya Yawe.
23Kisha watumishi wa Amoni walimwasi na kumwua katika nyumba yake ya kifalme.
24Lakini watu wa Yuda wakawaua wote waliomwua Amoni. Kisha watu hao wa Yuda wakamuweka mwana wake Yosia kuwa mufalme kwa pahali pake.
25Matendo mengine yote ya Amoni yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
26Amoni akazikwa katika kaburi katika bustani ya Uza. Yosia mwana wake akatawala kwa pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.