Kumbukumbu la Sheria 34 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kifo cha Musa

1Basi, Musa akaondoka kwenye bonde la Moabu, akaenda kwenye mulima Nebo, akapanda juu ya kilele cha Pisiga kinachoelekeana na Yeriko. Hapo Yawe akamwonyesha inchi yote: toka Gileadi mpaka Dani,

2eneo lote la Nafutali, eneo la Efuraimu na Manase, eneo lote la Yuda mpaka bahari ya Mediteranea,

3jangwa la Negebu na eneo la jangwa la bonde la Yeriko, muji wa miti ya ngazi mpaka Soari.

4Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”

5Basi, Musa mutumishi wa Yawe akakufa kule katika inchi ya Moabu kulingana na neno Yawe alilosema.

6Alizikwa katika bonde la Moabu, kuelekea muji wa Beti-Peori; lakini mpaka leo, hakuna mutu anayejua pahali alipozikwa.

7Musa alikuwa na umri wa miaka mia moja na makumi mbili alipokufa. Macho yake yalikuwa hayajafifia, na nguvu za mwili wake hazikupunguka.

8Waisraeli wakaomboleza kifo chake kwa muda wa siku makumi tatu kwenye inchi ya bonde la Moabu. Kisha siku za kilio na maombolezo ya kifo chake zikaisha.

9Yoshua mwana wa Nuni akajaa roho ya hekima, kwa sababu Musa alikuwa amemuwekea mikono yake. Hivyo Waisraeli wakamutii Yoshua na kufuata amri ambazo Yawe alimupa Musa.

10Hakujatokea tena nabii katika Israeli kama Musa, ambaye Yawe alisema naye uso kwa uso.

11Hakuna nabii mwingine ambaye alifanya vitambulisho na miujiza kama ile ambayo Yawe aliyomutuma Musa afanye mbele ya mufalme wa Misri, wakubwa wake na inchi yake yote.

12Hakuna nabii mwingine ambaye amefanya mambo makubwa na ya kutisha kama vile Musa alivyofanya mbele ya Waisraeli wote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help