1Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.
Wana wa Daudi2Wana ambao wake wa Daudi walimuzalia kule Hebroni walikuwa:
Amunoni muzaliwa wake wa kwanza, mama yake aliitwa Ahinoamu wa muji wa Yezereheli;
3Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli;
Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;
4Adonia muzaliwa wa ine, mama yake alikuwa Hagiti;
Sefatia muzaliwa wake wa tano, mama yake alikuwa Abitali;
5na Itiramu muzaliwa wake wa sita, mama yake alikuwa Egla, muke wa kwanza wa Daudi.
Wake wa Daudi walimuzalia wana hawa wote alipokuwa kule Hebroni.
Abeneri anajiunga na Daudi6Kadiri vita ilivyoendelea kati ya jamaa ya Daudi na ile ya Saulo, Abeneri alizidi kujiimarisha katika jamaa ya Saulo.
7Saulo alikuwa na habara mumoja aliyeitwa Risipa, binti ya Aya. Basi, wakati mumoja, Isiboseti akamwuliza Abeneri: “Kwa nini umelala na habara ya baba yangu?”
8Abeneri alikasirika sana kutokana na maneno ya Isiboseti, akasema: “Unafikiri mimi ni imbwa anayeitumikia jamaa ya Yuda? Angalia, mimi nimewatendea mema jamaa ya baba yako Saulo, wandugu zake, na warafiki zake na sikukutoa kwa Daudi mpaka leo. Hata hivyo, leo hii unaniona kuwa mwenye kosa kwa ajili ya mwanamuke.
9Mungu aniue ikiwa sitatimiza yote ambayo Yawe alimwapia Daudi.
10Yawe alimwapia Daudi kwamba atauhamisha ufalme kutoka jamaa ya Saulo na kumupa yeye. Naye atatawala inchi ya Israeli na Yuda kutokea Dani mpaka Beri-Seba.”
11Isiboseti hakuweza kusema neno, kwa sababu alikuwa anamwogopa Abeneri.
12Basi, Abeneri akatuma wajumbe kwa Daudi kule Hebroni wamwambie: “Inchi hii ni mali ya nani? Fanya agano na mimi, nami nitakusaidia kuifanya Israeli yote ikuwe chini yako.”
13Daudi akamujibu: “Ni vizuri, nitafanya agano nawe. Lakini ninakuomba jambo moja kwamba mbele haujaniona sharti kwanza uniletee Mikali binti ya Saulo. Hapo utaniona.”
14Daudi vilevile alituma wajumbe kwa Isiboseti mwana wa Saulo akisema: “Unirudishie muke wangu Mikali ambaye nilimwoa kwa magovi mia moja ya Wafilistini.”
15Basi, Isiboseti alituma watu, wakamukamata Mikali kutoka kwa mume wake Paltieli mwana wa Laisi.
16Lakini Paltieli akaenda pamoja na muke wake akiwa analia njia yote mpaka kule Bahurimu. Abeneri akamwambia Paltieli: “Rudia kwako.” Naye akarudi.
17Abeneri alifanya mashauri na wazee wa Waisraeli, akawaambia: “Kwa muda fulani uliopita mumekuwa mukitaka Daudi akuwe mufalme wenu.
18Sasa, mulilete jambo hilo mbele ya watu kwa sababu Yawe alimwahidi Daudi hivi: ‘Kwa mukono wako wewe Daudi mutumishi wangu, nitawaokoa watu wangu Waisraeli kutoka Wafilistini na kutoka waadui zao wengine.’ ”
19Abeneri akazungumuza na watu wa kabila la Benjamina, kisha akaenda mpaka Hebroni kumwambia Daudi juu ya yale ambayo watu wote wa Israeli na kabila lote la Benjamina walipatana kutenda.
20Abeneri alipomwendea Daudi, alikuwa na watu makumi mbili. Daudi aliwafanyia karamu.
21Abeneri akamwambia Daudi: “Mimi sasa nitakwenda na kukuletea watu wote wa Israeli, wewe bwana wangu mufalme. Watakuja na kufanya agano nawe, kusudi ukuwe mufalme wao, nawe utawatawala wote kama unavyopenda.” Daudi akamwaga Abeneri aende zake, naye akaondoka kwa amani.
Abeneri anauawa22Kisha, Yoabu pamoja na watu wa Daudi walirudi kutoka kwenye mashambulio, wakaleta vitu vingi. Lakini Abeneri hakukuwa pamoja na Daudi kule Hebroni maana Daudi alikuwa amemwaga aende zake, naye akaondoka kwa amani.
23Yoabu aliporudi akiwa na waaskari wake wote aliokuwa nao, aliambiwa kwamba Abeneri mwana wa Neri, alikuwa amekuja kumwona mufalme Daudi, naye amemwaga aende zake, naye ameondoka kwa amani.
24Yoabu alimwendea mufalme na kumwambia: “Sasa umefanya nini? Angalia Abeneri alikuja kwako; kwa nini umemwacha aende?
25Unajua kwamba Abeneri mwana wa Neri alikuja kukudanganya? Alikuja kusudi ajue mienendo yako na yale unayoyafanya.”
26Yoabu alipotoka kuzungumuza na Daudi, alituma wajumbe wamulete Abeneri, nao wakamukuta kwenye kisima cha Sira na kumurudisha, lakini Daudi hakujua jambo hilo.
27Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.
28Nyuma ya pale Daudi aliposikia habari hizo alisema: “Mimi na ufalme wangu hatuna kosa mbele ya Yawe juu ya damu ya Abeneri mwana wa Neri.
29Lazima ya mauaji hayo yakuwe juu ya kichwa cha Yoabu na jamaa yote ya baba yake! Jamaa ya Yoabu isikose mutu mwenye ugonjwa wa kisonono siku zote, au ugonjwa wa ukoma, au anayetembelea kwa miti au kuuawa kwa upanga, au mwenye kukosa chakula!”
30Yoabu na ndugu yake Abisayi walimwua Abeneri kwa sababu alikuwa amemwua ndugu yao Asaeli wakati wa vita kule Gibeoni.
31Kisha, mufalme Daudi akamwambia Yoabu na wale wote waliokuwa pamoja naye, wapasue nguo zao, wavae nguo ya gunia kusudi wafanye kilio kwa ajili ya Abeneri. Wakati wa mazishi hayo, mufalme Daudi alitembea nyuma ya kipoyi cha maiti ya Abeneri.
32Abeneri alizikwa kule Hebroni na mufalme aliomboleza kwa sauti akiwa pembeni ya kaburi. Watu wengine wote walifanya vile vile.
33Mufalme alimwomboleza Abeneri akisema:
“Imekufikia namna gani ee Abeneri kufa kama mupumbafu?
34Mikono yako haikufungwa
na miguu yako haikutiwa minyororo.
Amekufa kama mutu aliyeuawa na waovu!”
Na watu wote walimulilia tena.
35Kisha, watu wote walikwenda kumusihi Daudi akule chakula wakati ulipokuwa bado muchana. Lakini Daudi aliapa akawaambia: “Mungu aniue ikiwa nitaonja chakula au kitu chochote mpaka jua litakapotua.”
36Watu wote waliyaona mambo hayo, nao walipendezwa; kama vile kila kitu mufalme alichofanya kilivyowapendeza.
37Kwa hiyo, siku ile, Waisraeli wote walielewa kwamba haikukuwa nia ya mufalme Daudi kumwua Abeneri mwana wa Neri.
38Mufalme Daudi aliwaambia watumishi wake: “Hamujui kwamba leo mukubwa na mutu wa heshima amekufa katika inchi ya Israeli?
39Ijapokuwa mumenipakaa mafuta kusudi nikuwe mufalme, lakini leo mimi ni zaifu. Hawa wana wa Zeruya ni wakali kupita kipimo. Yawe awaazibu waovu hawa sawasawa na uovu wao.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.