1Mufalme Yosafati wa Yuda akarudi salama katika nyumba yake ya kifalme katika muji wa Yerusalema.
2Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.
3Lakini, kuna wema fulani ndani yako. Umekwisha kuondoa sanamu zote za Ashera, mungu wa kike, na umejikaza sana kumutafuta Mungu kwa moyo wote.”
Yosafati anafanya matengenezo4Mufalme Yosafati akakaa Yerusalema, lakini hata hivyo, mara kwa mara aliwatembelea watu wa Beri-Seba upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Efuraimu, upande wa kaskazini. Alifanya hivyo kwa kuwavuta watu wamurudilie Yawe, Mungu wa babu zao.
5Akaweka waamuzi katika miji yote ya Yuda yenye kuta,
6akawaambia: “Muwe waangalifu sana wakati munapoamua, kwa maana hukumu munayotoa hamuitoi kwa amri ya mwanadamu, lakini kwa amri inayotoka kwa Yawe, naye yuko pamoja nanyi munapotoa uamuzi.
7Basi, sasa mumwogope Yawe, mukuwe waangalifu katika kila jambo mutakalotenda kwa sababu Yawe wetu hatavumilia upotoshaji wa haki, wala upendeleo wala upokeaji wa kituliro.”
8Katika muji wa Yerusalema, Yosafati akaweka Walawi makuhani na wakubwa wa jamaa za Waisraeli wakuwe waamuzi wa magomvi yanayoelekea sheria za Yawe, au ugomvi kati ya wakaaji wa muji.
9Akawaamuru akisema: “Ndivyo mutakavyotenda mukimwogopa Yawe, kwa uaminifu na kwa moyo wote.
10Kila mara wandugu zenu kutoka katika muji wowote wanapowaletea mashitaki yoyote juu ya uuaji, kuvunja Sheria, amri, kanuni au maagizo, muwashaurie vema kusudi wasimukosee Yawe. Musipofanya hivyo, ninyi pamoja na wandugu zenu mutapatwa na kasirani ya Yawe. Lakini mukitenda vile, hamutakuwa na kosa.
11Amaria, Kuhani Mukubwa, ndiye atakayesimamia mambo yote yanayoelekea Yawe, naye Zebadia mwana wa Isimaeli, musimamizi wa inchi ya Yuda atasimamia mambo yote ya utawala, na Walawi watakuwa wakubwa. Mujipe moyo mutimize masharti haya, naye Yawe akuwe pamoja nao wanaokuwa wema.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.