Hesabu 28 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Sadaka za kila siku(Kut 29.38-46)

1Yawe akamwambia Musa:

2Uwaamuru Waisraeli maneno haya: Ninyi mutanitolea kwa wakati wake sadaka zinazotakiwa: vyakula vya kuteketezwa kwa moto, vyenye harufu nzuri ya kupendeza.

3Uwaambie kwamba sadaka watakayonitolea ya kuteketezwa kwa moto, itakuwa hii: wana-kondoo wawili wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema chochote, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.

4Mwana-kondoo mumoja atatolewa asubui na wa pili magaribi;

5kila mumoja atatolewa pamoja na sadaka ya vyakula ya kilo moja ya unga uliochanganywa pamoja na litre moja ya mafuta bora yaliyopondwa.

6Hii ni sadaka ya kutolewa kila siku inayoteketezwa kabisa kwa moto, ambayo ilitolewa kwa mara ya kwanza kwenye mulima Sinai kama sadaka ya ngano, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.

7Sadaka ya kinywaji itakayotolewa na kila mwana-kondoo ni litre moja ya divai. Utaimimina sadaka hii ya kinywaji kikali Pahali Patakatifu.

8Wakati wa magaribi utamutoa yule mwana-kondoo mwingine kwa kuteketezwa kwa moto, pamoja na sadaka zile za ngano na za kinywaji. Itakuwa sadaka yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.

Sadaka za Sabato

9Siku ya Sabato, mutatoa sadaka ya wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema, sadaka ya vyakula ya kilo mbili za unga laini uliochanganywa na mafuta, na sadaka yake ya kinywaji.

10Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa kila siku ya Sabato zaidi ya ile sadaka ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.

Sadaka za kila mwezi

11Kwa mwanzo wa kila mwezi, mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.

12Mutatoa sadaka ya vyakula ya unga laini kilo tatu, uliochanganywa na mafuta kwa kila ngombe dume mumoja; mutatoa kilo mbili za unga; kwa kila kondoo dume,

13na kilo moja ya unga kwa kila mwana-kondoo. Sadaka hizi za kuteketezwa ni sadaka za chakula zenye harufu ya kumupendeza Yawe.

14Kipimo cha sadaka ya kinywaji kinachohitajika ni litre mbili za divai kwa kila ngombe dume; litre moja na nusu kwa kila kondoo dume, na litre moja kwa kila mwana-kondoo. Hii ndiyo sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi katika mwaka muzima.

15Tena mutamutolea Yawe sadaka kwa ajili ya zambi, beberu mumoja, zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji.

Sadaka za Pasaka(Law 23.5-14)

16Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza ni Pasaka ya Yawe. Ang. Kut 12.1-13; Kumb 16.1-2

17Siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni sikukuu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu. Ang. Kut 12.14-20; 23.15; 34.18; Kumb 16.3-8

18Katika siku ya kwanza kutakuwa mukutano mutakatifu. Siku hiyo hamutafanya kazi.

19Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kama vile sadaka ya ngano kwa Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe bila kilema.

20Sadaka ya ngano itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta, kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume,

21na kilo moja kwa kila mumoja wa wale wana-kondoo saba.

22Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.

23Mutatolea vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida inayotolewa kila siku asubui.

24Vivyo hivyo, kwa muda wa siku saba, mutatoa kila siku sadaka ya ngano ya kuteketezwa. Itakuwa ni harufu nzuri ya kumupendeza Yawe. Hii mutaitoa zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji.

25Katika siku ya saba mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi.

Sadaka ya sikukuu ya mavuno(Law 23.15-22)

26Katika siku ya kwanza ya sikukuu ya majuma wakati munapomutolea Yawe malimbuko ya ngano zenu, mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi.

27Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote hao wakuwe bila kilema.

28Sadaka ya ngano itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume,

29na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

30Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.

31Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya kinywaji.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help