Waebrania 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yesu, Kuhani wetu Mukubwa

1Jambo la lazima sana katika maneno tunayosema sasa ni hili. Tuko na Mukubwa wa namna ile, anayeikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mwenyezi Mungu.

2Yeye anafanya kazi ya Kuhani Mukubwa katika Pahali Patakatifu Sana, maana yake katika hema ya kweli iliyosimikwa na Bwana, wala si mutu.

3Kila Kuhani Mukubwa anawekwa kusudi afanye kazi ya kutoa sadaka na matoleo. Kufuatana na hiyo, ilimupasa Kuhani wetu Mukubwa Kristo akuwe na kitu cha kutoa vilevile.

4Kama Kristo angekuwa katika dunia, asingekuwa kuhani hata kidogo, kwa sababu kuko makuhani wanaotoa sadaka kufuatana na maagizo ya Sheria.

5Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”

6Lakini sasa Yesu amepewa kazi inayokuwa bora zaidi kuliko kazi ya wale makuhani, kwa maana yeye ni mupatanishi wa agano linalokuwa zuri zaidi. Sherti za agano lile zinasimamia juu ya ahadi ya Mungu inayokuwa bora zaidi.

7Kama lile agano la kwanza lingekuwa kamilifu, haingekuwa lazima likombolewe na la pili.

8Lakini Mungu aliwaonya watu wake, akisema:

“Katika siku zinazokuja,

nitafanya agano jipya na watu wa ufalme wa Israeli

na wa Yuda.

Ni Bwana anayesema hivyo.

9Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao

siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri.

Kwa sababu hawakushika lile agano,

kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia.

Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.

10Sasa hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa ufalme wa Israeli

katika siku zile:

nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri yao,

nikiziandika ndani ya mioyo yao.

Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.

Nitakuwa Mungu wao,

nao watakuwa watu wangu.

11Hakutakuwa tena atakayefundisha mwanainchi mwenzake, au kumwambia ndugu yake:

‘Umujue Bwana.’

Kwa maana watu wote watanijua,

tangu mudogo mpaka mukubwa.

12Mimi nitawasamehe maovu yao,

wala sitakumbuka tena zambi zao.”

13Mungu alipotangaza hilo agano kuwa “jipya”, jambo hilo lilisababisha lile la kwanza kuwa la zamani na lenye kuchakaa. Na kitu chochote kikiwa cha zamani na chenye kuchakaa kinafikia wakati wa kutoweka.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help