1Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu,
lakini kwa moyo wako ushike amri zangu.
2Maana vitakupa wingi wa siku,
maisha marefu na fanaka kwa wingi.
3Wema na uaminifu zisitengane nawe.
Uvifunge katika shingo lako;
uviandike ndani ya moyo wako.
4Hivyo utakubaliwa na kusifiwa,
mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.
5Umutumainie Yawe kwa moyo wako wote,
wala usitegemee akili zako mwenyewe.
6Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya,
naye atasawanisha njia zako.
7Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima;
umwogope Yawe na kujiepusha na uovu.
8Hiyo itakuwa dawa kwa mwili wako,
na kitu cha kutuliza mifupa yako.
9Umuheshimu Yawe kwa mali yako,
na kwa malimbuko ya mazao yako yote.
10Kwa hiyo gala zako zitajaa ngano,
na mitungi yako itafurika na divai mupya.
11Mwana wangu, usizarau azabu ya Yawe,
wala usiuzike kwa maonyo yake;
12maana Yawe anaonya yule anayemupenda,
kama vile baba anavyomwonya mwana wake mupenzi.
13Heri mutu anayetambua hekima,
mutu yule anayepata ufahamu.
14Hekima ni bora kuliko feza,
ina faida kuliko zahabu.
15Hekima ni ya maana sana kuliko mawe ya bei kali,
hakuna kitu unachotamani kinachoweza kulingana nayo.
16Itakupa maisha marefu,
mali na heshima.
17Njia zake ni za kupendeza,
zote zinaelekea kwenye amani.
18Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata;
wana heri wote wanaoshikamana nayo.
19Kwa hekima Yawe aliweka misingi ya dunia,
kwa akili aliziimarisha mbingu.
20Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka,
na mawingu yakadondosha umande.
21Mwana wangu, shika hekima safi na akili;
usiviache vitoweke mbele ya macho yako,
22navyo vitakuwa uzima katika nafsi yako,
na pambo zuri katika shingo lako.
23Halafu utaweza kwenda zako kwa usalama,
wala muguu wako hautajikwaa.
24Unapolala, hautakuwa na hofu,
utapata usingizi muzuri.
25Usiogope juu ya tisho la rafla,
wala shambulio kutoka kwa waovu,
26maana Yawe ndiye atakayekutegemeza,
atakuepusha usipate kunaswa katika mutego.
27Usimunyime mutu anayehitaji musaada,
ikiwa una uwezo wa kufanya hivyo.
28Usimwambie jirani yako
“Kwenda na urudie kesho, halafu nitakupatia”
wakati wewe unaweza kumupa anachohitaji leo.
29Usipange maovu juu ya jirani yako
anayeishi karibu nawe bila wasiwasi.
30Usigombane na mutu bila sababu,
ikiwa hajakuzuru kwa lolote.
31Usimwonee wivu mutesaji,
wala usiige mwenendo wake.
32Maana waovu ni chukizo kwa Yawe,
yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.
33Yawe analaani nyumba za waovu,
lakini anabariki makao ya wenye haki.
34Yeye anazarau wenye mazarau,
lakini anakubali wanyenyekevu.
35Wenye hekima watavuna heshima,
lakini wapumbafu watapata haya.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.