1Ninyi wake, muwatii waume wenu, kusudi kukiwa wamoja kati yao wasioamini neno la Mungu, mupate kuwavuta kwa kulisadiki kwa mwenendo wenu muzuri pasipo kuwaambia neno.
2Wataweza kuvutwa kwa kuona mwenendo wenu safi na wa heshima.
3Kujipamba kwenu kusikuwe kwa inje sawa vile kusuka nywele, kuvaa mapambo ya zahabu au nguo za bei kali.
4Lakini mapambo yenu yanapaswa kuwa ya ndani ya moyo yasiyoweza kuharibika. Sherti mapambo yale yakuwe yenye kutokana na roho ya amani na upole inayohesabiwa kuwa ya bei kali mbele ya Mungu.
5Kwa maana ni vile ndivyo wanawake waliomwabudu Mungu kwa kweli na kumutumainia walivyojipamba wakiishi katika utii mbele ya waume wao.
6Ni vile Sara alimutii Abrahamu, akimwita “Bwana.” Ninyi ni wabinti zake kama mukifanya mema pasipo kuogopa kitisho chochote.
7Vilevile, ninyi waume, mukae na wake wenu mukifahamu kwamba wao ni kiumbe kizaifu. Munapaswa vilevile kuwapa heshima kwa sababu watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima. Mufanye hivi kusudi maombi yenu yasizuizwe.
Kuteswa kwa ajili ya haki8Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.
9Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.
10Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema:
“Kuna mutu anayependa kuishi vizuri, na kukaa katika siku za heri?
Azuize ulimi wake na mabaya nayo midomo yake na uongo.
11Aepuke mabaya, atende mema,
atafute amani na kuifuatilia.
12Kwa maana macho ya Bwana yanawaelekea wenye haki,
nayo masikio yake yanasikiliza maombi yao.
Lakini uso wa Bwana unawapinga waovu.”
13Ni nani atakayewazuru ninyi kama mukiwa wenye bidii katika kutenda mema?
14Hata mukiteswa kwa ajili ya haki, ninyi ni wenye heri. Musiwaogope watu, wala musihangaike.
15Lakini mumutukuze Bwana wenu Kristo ndani ya mioyo yenu. Mukuwe tayari wakati wowote kumujibu kila mutu anayewauliza juu ya tumaini munalokuwa nalo. Lakini mufanye vile kwa upole na heshima,
16mukiwa na zamiri safi, hata wale wanaowasingizia na kuwatukana juu ya mwenendo wenu muzuri katika ushirika wenu na Kristo, wapate haya.
17Kwa maana kuteswa kwa ajili ya kutenda mema, ikiwa ni mapenzi ya Mungu, ni vizuri kuliko kuteswa kwa ajili ya kutenda mabaya.
18Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.
19Kwa njia ya huyu Roho alienda hata kuhubiri roho zilizokuwa katika kifungo.
20Roho zile ni za watu walioasi Mungu zamani za kale alipowavumilia katika siku Noa alipotengeneza chombo kikubwa. Ni watu wanane tu ndio waliingia ndani ya chombo na kuokolewa katika maji.
21Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,
22aliyepanda mbinguni, na anayekaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, akitawala wamalaika, nao wenye mamlaka na uwezo wanaokuwa katika mbingu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.