Isaya 18 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu ataiazibu inchi ya Kushi

1Ole, kwa inchi iliyojaa muvumo wa mabawa,

inchi inayokuwa ngambo ya mito ya Kushi!

2Inatuma wajumbe ambao wanasafiri ndani ya muto Nili,

wamepanda ndani ya mitumbwi iliyotengenezwa na matete.

Muende, enyi wajumbe wepesi,

kwa taifa kubwa na hodari,

la watu warefu wenye ngozi laini,

wanaotisha kwa karibu na kwa mbali,

taifa la watu wenye nguvu na ushindi,

ambalo inchi yake imegawanywa na mito.

3Enyi wakaaji wote katika ulimwengu,

nanyi munaojaza dunia!

Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie!

Baragumu itakapopigwa, musikilize.

4Maana, Yawe ameniambia hivi:

Tokea juu kwenye makao yangu nitaangalia yanayotukia,

nikitulia kama joto katika mwangaza wa jua,

kama wingu la umande wakati wa mavuno.

5Maana, mbele ya mavuno, wakati wa kuchanua umekwisha,

maua yameanguka na kuwa zabibu yenye kukomaa,

Mungu atakata chipukizi kwa upanga,

na kuyakwanyua matawi.

6Yote yataachiwa ndege wa milima

na nyama wengine wa pori.

Ndege wakali watakaa humo

wakati wa jua,

na nyama wa pori watafanya makao humo

wakati wa baridi.

7Wakati huo, Yawe wa majeshi ataletewa sadaka kutoka kwa watu warefu na wenye ngozi laini, watu wanaotisha kwa karibu na kwa mbali, taifa la watu wenye nguvu na ushindi, ambalo inchi yake imegawanywa na mito. Ataletewa sadaka hizo kwenye mulima Sayuni anapoabudiwa yeye Yawe wa majeshi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help