Mezali 30 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maneno ya Aguri

1Maneno ya Aguri mwana wa Yake. Maneno ambayo mutu huyu alimwambia Itieli na Ukali.

2Mimi ni mupumbafu sana, wala si mutu;

sina akili ya mwanadamu.

3Sijajifunza hekima,

wala sijui kitu juu ya Mungu Mutakatifu.

4Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini?

Ni nani aliyekamata upepo katika mukono?

Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa?

Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia?

Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake?

Uniambie kama unajua!

5Maneno yote ya Mungu ni ya kuaminiwa.

Yeye ni ngao yao wote wanaomukimbilia.

6Usiongeze neno katika maneno yake,

kusudi asikukaripie, nawe usionekane kuwa mwongo.

7Ee Mungu, ninakuomba mambo haya mawili,

wala usikatae kunitimizia nayo mbele ya kufa kwangu:

8Uniondolee uongo na udanganyifu;

usinipe umasikini wala utajiri;

unipatie chakula ninachohitaji,

9maana nikipata mali mengi nitakusahau;

nikisema: “Yawe ni nani?”

Au nikiwa masikini nitaiba,

na kuzaraulisha jina lako ee Mungu wangu.

10Usimuchongee mutumwa kwa bwana wake,

kusudi asikulaani, na kuonekana kwamba uko na kosa.

11Kuna watu ambao wanalaani baba zao,

wala hawana shukrani kwa mama zao.

12Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi,

kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.

13Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi.

Wanazarau kila kitu wanachoona.

14Kuna watu ambao meno yao ni kama upanga,

na mataya yao ni kama visu.

Wako tayari kuwatafuna wamasikini wa inchi,

na wakosefu wanaokuwa kati ya watu!

15Muruba ana wabinti wawili wanaosema: “Unipe, Unipe!”

Kuna vitu vitatu ambavyo havishibi hata kidogo,

hata vitu vine visivyosema: “Inatosha!”

16Kuzimu,

tumbo la mwanamuke tasa,

udongo usioshiba maji,

na moto usiosema: “Inatosha!”

17Kama mutu akimuchekelea baba yake

na kuzarau utii kwa mama yake,

macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori

na kuliwa na tai.

18Kuna mambo matatu yanayokuwa ya ajabu kwangu,

hata mambo mane nisiyoyaelewa:

19njia ya tai katika anga,

njia ya nyoka juu ya jiwe,

njia ya mashua ndani ya bahari,

na njia ya mwanaume kwa mwanamuke.

20Mwenendo wa mwanamuke mwasherati ni hivi:

yeye anakula, anajipanguza mudomo,

na kusema: “Sijafanya kosa lolote!”

21Kuna mambo matatu ambayo yanaitetemesha dunia,

hata mambo mane ambayo haiwezi kuyavumilia:

22mutumwa anayekuwa mufalme;

mupumbafu anayeshiba chakula;

23mwanamuke asiyependwa anayeolewa;

na mujakazi anapotwaa nafasi ya bibi yake.

24Kuna viumbe vine vidogo sana katika dunia,

lakini vina akili sana:

25siafu ni wadudu wasiokuwa na nguvu,

lakini wanajiwekea chakula wakati wa kipwa;

26sungura ni nyama wasiokuwa na uwezo,

lakini wanajitengenezea makao chini ya mawe;

27nzige hawana mufalme,

lakini wote wanaenda pamoja kwa vikundi;

28mujusi, unaweza kumushika katika mukono,

lakini anaingia katika nyumba ya kifalme.

29Kuna viumbe vitatu vyenye mwendo wa kupendeza,

hata viumbe vine vyenye mwendo muzuri:

30simba, ambaye ni nyama mwenye nguvu kuliko wote wala hamwogopi nyama mwingine yeyote,

31jogoo anayetembea kwa maringo,

beberu,

na mufalme mbele ya watu wake.

32Kama umekuwa mupumbafu hata ukajisifu,

au kama umekuwa unapanga maovu,

chunga mudomo wako.

33Maana ukigandisha maziwa, utapata siagi;

ukimupiga mutu kwenye pua, atatoka damu.

Vilevile kuchochea hasira kunaleta ugomvi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help