1Kisha makabila yote ya Waisraeli yalimwendea Daudi kule Hebroni, na kumwambia: “Angalia, sisi ni mwili na damu yako.
2Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”
3Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.
4Daudi alikuwa na umri wa miaka makumi tatu alipoanza kutawala, na alitawala kwa muda wa miaka makumi ine.
5Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.
6Kisha mufalme na watu wake walikwenda Yerusalema kuwashambulia Wayebusi waliokuwa wenyeji wa inchi hiyo. Lakini wao wakamwambia: “Hautaingia ndani ya muji huu, maana vipofu na vilema watakufukuza.” Walimwambia hivyo maana walifikiri kwamba Daudi asingeweza kuingia katika muji ule.
7Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.
8Siku hiyo, Daudi alisema: “Mutu yeyote atakayewapiga Wayebusi apitie kwenye mufereji wa maji kwa kuwashambulia vilema na vipofu ambao roho yangu inawachukia.” Ndiyo maana watu wanasema: “Vipofu na vilema hawataingia katika nyumba.”
9Daudi alikaa kwenye kikingio hicho. Akakiita: “Muji wa Daudi.” Daudi akaongeza muji, akianzia uwanja wa Milo kuelekea ndani.
10Naye Daudi akazidi kuwa na uwezo zaidi kwa sababu Yawe, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.
11Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.
12Hivyo, Daudi akatambua kwamba Yawe amemwimarisha akuwe mufalme wa Israeli, na kwamba ameutukuza ufalme wake kwa ajili ya watu wake Waisraeli.
13Daudi alijitwalia wahabara na kuoa wake zaidi wa kule katika muji wa Yerusalema kisha kutoka Hebroni. Hao, wakamuzalia wana na wabinti.
14Haya ndiyo majina ya wana ambao wake zake walimuzalia kule Yerusalema: Samua, Sobabu, Natani, Solomono,
15Ibuhari, Elisua, Nefegi, Yafia,
16Elisama, Eliada na Elifeleti.
Ushindi juu ya Wafilistini(1 Sik 14.8-17)17Wafilistini waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mufalme wa Waisraeli, wote walitoka kwenda kumutafuta, lakini yeye alipata habari, akaingia ndani ya makimbilio.
18Wafilistini walifika na kujitawanya kwenye Bonde la Refaimu.
19Basi, Daudi alimwuliza Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?”
Naye Yawe akamwambia Daudi: “Kwenda, maana hakika nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”
20Basi, Daudi akafika Bali-Perasimu na kuwashinda Wafilistini. Halafu akasema: “Yawe amepita katikati ya waadui zangu kama mafuriko ya maji yanayoenda mbio.” Kwa hiyo pahali pale pakaitwa “Bwana Anayepita Katikati”.
21Wafilistini waliziacha sanamu zao za miungu pahali pale, naye Daudi na watu wake wakazikamata.
22Kwa mara ya pili, Wafilistini walifika tena na kujitawanya kwenye bonde la Refaimu.
23Daudi alipomwomba Yawe shauri, Yawe alimwambia: “Usiwashambulie kutoka hapa unapokuwa, lakini zunguka nyuma yao na kuwashambulia kutokea mbele ya miti ya miforosadi.
24Na mara moja mutakaposikia vishindo vya miguu kwenye vilele vya miforosadi hiyo, halafu ujipe moyo maana nitakuwa nimetoka kwa kukutangulia kuwapiga waaskari wa Wafilistini.”
25Daudi alifanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe, naye akawapiga Wafilistini kutokea Geba mpaka Gezeri.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.