1Daudi akashauriana na majemadari wa makundi ya maelfu na makundi ya mamia, pamoja na viongozi wote.
2Kisha akawaambia Waisraeli wote waliokusanyika: “Ikiwa mutakubaliana nami, na ikiwa ni mapenzi ya Yawe, Mungu wetu, tufanye hivi: tutume wajumbe waende wawaite wandugu zetu waliobaki katika inchi ya Israeli, pamoja na makuhani na Walawi wanaokuwa katika miji yao na mashamba ya malisho yao, wakuje kukusanyika pamoja nasi.
3Kisha tuende tukamate Sanduku la Agano la Mungu wetu, maana hatukulijali wakati wa utawala wa mufalme Saulo.”
4Watu wote wakakubaliana na pendekezo lile maana waliliona kuwa jambo jema.
5Kwa hiyo, Daudi akawakusanya Waisraeli wote katika inchi, tokea kwenye kijito cha Sihori kinachokuwa Misri, mpaka kwenye kiingilio cha Hamati kwa kulileta Sanduku la Agano toka Kiriati-Yearimu. lakini akalipeleka katika nyumba ya Obedi-Edomu wa Gati.
14Sanduku lile la Mungu lilikaa kule kwa Obedi-Edomu kwa muda wa miezi mitatu, naye Yawe akabariki nyumba ya Obedi-Edomu na mali yake yote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.