1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi.
2Enyi watawala, munasema kwa haki kweli?
Munawahukumu watu kwa usawa?
3Hapana. Ninyi munafikiria tu kutenda maovu;
ninyi wenyewe munaeneza mateso makali katika inchi.
4Waovu wamepotoka tangu kuzaliwa kwao,
hao waongo wamekosa tangu walipozaliwa.
5Wana sumu kama sumu ya nyoka.
Wao ni viziwi kama piri anayeziba masikio,
6ambaye hasikii hata sauti ya mulozi,
au ya muganga anayekuwa fundi wa uchawi.
7Ee Mungu, uvunje meno yao,
uongoe, ee Yawe, meno ya simba wakali hao.
8Watoweke kama maji yanavyopotelea ndani ya muchanga,
kama majani wakanyagwe na kunyauka,
9watoweke kama konokono anavyoyeyuka akitembea,
kama mimba iliyoharibika isiyoona jua hata kidogo!
10Mbele hawajatambua, waongolewe
kama miiba, michongoma au magugu.
Kwa hasira ya Mungu, wapeperushwe mbali,
wakikuwa bado wazima.
11Watu wa haki watafurahi wanapoona waovu wanaazibiwa;
watatembea katika damu ya watu wabaya.
12Watu wote watasema:
“Kweli, watu wa haki wanapata zawadi!
Hakika, kuna Mungu anayehukumu dunia!”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.