1Musa akamwambia Mungu: “Lakini Waisraeli hawataniamini wala kunisikiliza. Watasema kwamba wewe Yawe haukunitokea.”
2Yawe akamwambia Musa: “Unashika nini katika mukono wako?”
Musa akamwambia: “Fimbo.”
3Yawe akamwambia: “Uitupe chini.” Musa akatupa fimbo chini, nayo ikageuka kuwa nyoka. Musa akaikimbia.
4Lakini Yawe akamwambia Musa: “Nyoosha mukono wako, uikamate mukia!” Musa akanyoosha mukono wake, akaikamata na nyoka ikageuka tena kuwa fimbo katika mukono wake.
5Yawe akamwambia: “Hivyo Waisraeli watapata kuamini kwamba mimi Yawe, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, nimekutokea.”
6Tena, Yawe akamwambia Musa: “Ingiza mukono wako kwenye kifua chako.” Musa akafanya hivyo. Alipoutoa inje, ukakuwa na ukoma, mweupe kama teluji.
7Kisha Mungu akamwambia: “Ingiza tena mukono wako kwenye kifua chako!” Musa akaingiza mukono wake kwenye kifua. Alipoutoa inje, ukarudilia hali yake ya kawaida kama vile mwili wake unavyokuwa.
8Mungu akamwambia Musa: “Wasipokuamini au kusadiki kitambulisho cha kwanza, inawezekana wataamini kitambulisho cha pili.
9Lakini wasipoamini hata vitambulisho hivi viwili, au kuamini maneno yako, utachota maji ya muto Nili na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Maji hayo yatakuwa damu juu ya inchi kavu.”
10Lakini Musa akamwambia Yawe: “Ewe Bwana wangu, mimi mutumishi wako sina ufundi wa kusema tangu zamani, hata kisha kusema nawe. Ulimi wangu ni muzito.”
11Halafu Yawe akamwuliza: “Ni nani aliyeumba kinywa cha mutu? Ni nani anayemufanya mutu kuwa bubu au kiziwi? Aone au akuwe kipofu? Si mimi Yawe?
12Basi, kwenda! Mimi nitaongoza kinywa chako na kukufundisha cha kusema.”
13Lakini Musa akasema: “Ee Bwana wangu, tafazali ninakusihi, umutume mutu mwingine.”
14Halafu hasira ya Mungu ikawaka juu ya Musa, akamwambia: “Si kuna ndugu yako Haruni ambaye ni Mulawi? Ninajua yeye anajua kusema vizuri. Tena anakuja kukutana nawe, na mara tu atakapokuona atafurahi ndani ya moyo.
15Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidia na kuwafundisha mambo mutakayofanya.
16Haruni ataongea na Waisraeli kwa ajili yako. Yeye atakuwa musemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.
17Utatwaa katika mukono wako fimbo hii ambayo utaitumia kufanya vile vitambulisho.”
Musa anarudi Misri18Musa akarudi kwa Yetro, baba mukwe wake, akamwambia: “Tafazali uniruhusu nirudie Misri kwa wandugu zangu, nione kama wangali wazima.” Yetro akamwambia: “Kwenda kwa amani.”
19Musa akiwa bado katika inchi ya Midiani, Yawe akamwambia: “Rudi Misri kwa sababu wale wote waliotaka kukuua wamekwisha kufa.”
20Basi, Musa akatwaa muke wake na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Katika mukono wake alishika ile fimbo aliyoamuriwa na Mungu aitwae.
21Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.
22Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.
23Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”
24Akiwa bado katika njia kurudi Misri, Musa alikuwa pahali pa kulala pa wageni. Basi, Mungu akakutana naye na kutaka kumwua.
25Kwa hiyo Zipora akakimbia haraka, akatwaa jiwe kali, akakata govi la mwana wake na kumugusa nalo Musa kwenye miguu akisema: “Wewe ni bwana-arusi wa damu.”
26Kwa hiyo Yawe akamwacha Musa. Zipora alikuwa amesema: “Bwana-arusi wa damu”, kwa sababu ya kutahiri.
27Yawe akamwambia Haruni: “Kwenda katika jangwa ukutane na Musa.” Basi, Haruni akaenda, akakutana na Musa kwenye mulima wa Mungu, akamubusu.
28Naye Musa akamwambia Haruni maneno yote aliyoambiwa na Yawe ayaseme na vitambulisho vyote alivyoagizwa atende.
29Kisha Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli.
30Haruni akawaambia maneno yote Yawe aliyokuwa amemwagiza Musa na kufanya vile vitambulisho mbele ya watu wote.
31Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.