1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo, na kwa ndugu yetu Timoteo. Tunakuandikia wewe Filemono, mupendwa wetu na mwenzetu wa kazi,
2na kanisa linalokusanyika katika nyumba yako, na dada yetu Apia na Arkipo mupiganaji mwenzetu wa vita.
3Tunawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Upendo na imani ya Filemono4Ninamushukuru Mungu wangu siku zote nikikukumbuka wewe Filemono katika maombi yangu.
5Kwa maana ninasikia namna unavyomwamini Bwana Yesu na namna unavyowapenda watu wote wa Mungu.
6Ninamwomba Mungu kwamba ushirika wa imani yako uzae matunda, na kwa njia hiyo upate kujua mema yote tunayokuwa nayo katika kuungana kwetu na Kristo.
7Ndugu, upendo wako umenifurahisha sana na kunifariji, kwa maana umetuliza mioyo ya watu wa Mungu.
Paulo anamwombea Onesimo8Kwa sababu hii, ingawa ninakuwa na mamlaka niliyopewa na Kristo kukuagiza neno unalopaswa kufanya,
9lakini kwa ajili ya upendo, ninapendelea kukusihi, mimi Paulo ninayekuwa muzee, na zaidi sasa ninakuwa mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo.
10Ninakusihi kwa ajili ya mutoto wangu Onesimo, niliyemuzaa katika imani nikiwa katika kifungo.
11Zamani yeye hakukufalia kitu, lakini sasa atakufalia wewe na mimi vilevile.
Maagizo na salamu za mwisho12Sasa ninamurudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13Ningalipenda Onesimo abakie pamoja nami kwa kunisaidia pahali pako wakati ninapokuwa mufungwa kwa sababu ya Habari Njema.
14Lakini sikutaka kufanya kitu chochote pasipo shauri lako. Wala sikutaka kukulazimisha unitendee mema; lakini ningetaka uyatende kwa mapenzi yako mwenyewe.
15Labda hii ndiyo sababu Onesimo aliachana nawe kwa muda, kusudi upate tena kuwa naye siku zote.
16Kwa sababu sasa yeye si kama vile mutumwa tu, lakini amekuwa bora zaidi kuliko mutumwa: yeye ni ndugu mupendwa. Mimi ninamupenda sana, nawe utamupenda zaidi sana, kwanza kama vile mutumwa, tena kama vile ndugu katika Bwana.
17Basi kama unaendelea kunihesabu kuwa mwenzako, umupokee kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18Kama alikukosea au kama yuko na deni yako ya kitu chochote, unidai mimi.
19Mimi Paulo ninaandika kwa mukono wangu mwenyewe maneno haya: nitakulipa. (Sitaki kusema kwamba maisha yako ni deni unalokuwa nalo kwangu.)
20Ndiyo, ndugu yangu, ninakusihi unisaidie kwa njia hii kwa ajili ya Bwana, unitulize moyo kama vile ndugu katika Kristo.
21Ninapokuandikia, nina uhakika kwamba utanisikia na hata utafanya zaidi kuliko vile nilivyosema.
22Lakini pamoja na maneno haya, unitayarishie vilevile pahali pa kukaa, maana ninatumaini kwamba Mungu atajibu maombi yenu, na kunijalia nipate kurudishwa tena kwenu.
23Epafra, mufungwa mwenzangu, kwa ajili ya Yesu Kristo, anakusalimia.
24Vilevile Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanya kazi wenzangu, wanakusalimia.
25Ninawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.