1Nyuma ya mambo yale, hasira yake ilipokwisha kutulia, mufalme Ahasuero akamukumbuka Vashiti, akakuwa anafikiri juu ya ugumu wake na hatua iliyokamatwa juu yake.
2Basi, watumishi wake, waliokuwa wanamutumikia yeye peke yake, wakamushauria: “Wamutafutie mufalme wabinti wazuri ambao ni mabikira.
3Mufalme achague wakubwa katika kila jimbo la utawala wake, na kuwaagiza wawalete wabinti wote wazuri ambao ni mabikira kwenye nyumba ya wanawake hapa Susani, muji mukubwa. Halafu wawekwe chini ya uangalizi wa Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wako; na hapo wapewe mafuta na vifaa vingine kusudi wajipambe zaidi.
4Yule atakayekupendeza zaidi, afanywe malkia pahali pa Vashiti.” Mufalme akaona shauri hilo ni jema, akafanya hivyo.
5Katika muji wa Susani, kulikuwa mutu mumoja Muyuda, jina lake Mordekayi, mwana wa Yairi wa uzao wa Simei, na Kisi wa kabila la Benjamina.
6Mordekayi alikuwa kati ya watu wale waliopelekwa kuwa wafungwa wakati mufalme Yekonia wa Yuda alipotekwa na mufalme Nebukadneza wa Babeli.
7Alikuwa anamulea binamu yake Hadasa ndiye Esteri. Esteri alikuwa binti muzuri wa sura na umbo. Wazazi wake walipokufa, Mordekayi akamutwaa Esteri, akamulea kama binti yake.
8Amri ya mufalme ilipotangazwa, wabinti wengi wakapelekwa Susani, muji mukubwa, wakawekwa chini ya ulinzi wa Hegayi. Esteri naye, akapelekwa kwenye nyumba ya kifalme, akawekwa chini ya uangalizi wa Hegayi, yule mwangalizi wa wanawake.
9Hegayi akapendezwa na Esteri hata kiasi cha kumupendelea. Bila kupoteza wakati, akamupa Esteri mafuta na chakula. Vilevile, akamuhamishia pahali pazuri kabisa katika nyumba hiyo ya wanawake, akamuchagulia wajakazi saba kutoka nyumba ya mufalme.
10Esteri alikuwa hajatambulisha ukoo wala kabila lake, maana Mordekayi alikuwa amemwonya asifanye hivyo.
11Kila siku Mordekayi alipitapita mbele ya kiwanja cha nyumba hiyo ya wanawake kusudi apate kujua hali ya Esteri na mambo ambayo yangemupata.
12Kipindi cha hao wabinti kwa kujipodoa na kujitia uzuri kilikuwa mwaka mumoja: miezi sita ya kwanza walitumia mafuta ya manemane, na miezi sita ya mwisho walitumia marasi na mafuta mengine. Nyuma ya pale, kila binti, peke yake, alipelekwa kwa mufalme Ahasuero.
13Wakati wa kwenda kwa mufalme, kila binti alipewa kila kitu alichotaka kutwaa kutoka nyumba ya wanawake kwenda nacho katika nyumba ya kifalme.
14Magaribi ulikuwa ndio wakati wa kwenda, na kesho yake asubui, binti huyo alipelekwa katika nyumba nyingine ya wanawake, chini ya uongozi wa Sasagazi, towashi musimamizi wa wahabara wa mufalme. Binti hakupaswa kurudi kwa mufalme, isipokuwa kama mufalme amependezwa naye, na aliitwa kwa jina.
15Wakati ukafika wa Esteri kwenda kwa mufalme. Huyo, binti wa marehemu Abihaili, binamu ya Mordekayi, na ambaye alilelewa na Mordekayi, hakuomba kitu chochote zaidi ya kile alichopangiwa na Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wa mufalme. Esteri akapata kukubaliwa mbele ya kila mutu aliyemwona.
16Basi, Esteri akapelekwa katika nyumba kwa mufalme katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Ahasuero, mwezi wa kumi unaoitwa Tebeti.
17Mufalme akamupenda zaidi Esteri kuliko wanawake wote. Naye Esteri akapata kukubaliwa na kutendewa mema mbele yake zaidi kuliko wabinti wengine wote. Basi, mufalme akamuvalisha taji ya kimalkia kwenye kichwa, akamufanya malkia pahali pa Vashiti.
18Kisha mufalme akafanya karamu kubwa kwa heshima ya Esteri, akawaalika viongozi na watumishi wote wa serikali yake. Vilevile, mufalme akatangaza musamaha wa kodi katika majimbo yote, akatoa zawadi nyingi kulingana na mapato yake ya kifalme.
Mordekayi anaokoa maisha ya mufalme19Wabinti walipokusanyika mara ya pili, Mordekayi alikuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme.
20Esteri alikuwa bado hajatambulisha ukoo wala kabila lake kama vile Mordekayi alivyokuwa amemwonya asifanye. Naye Esteri akamutii kama alivyokuwa akimutii wakati wa utoto wake, alipolelewa naye.
21Wakati Mordekayi alipokuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme, Bigitani na Teresi, wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa milango ya vyumba vya mufalme, walikasirika hata wakafanya shauri baya la kumwua mufalme Ahasuero.
22Mordekayi akapata habari hiyo, akamujulisha malkia Esteri, naye Esteri akamupasha mufalme habari.
23Uchunguzi ulipofanywa, iligunduliwa kwamba ni kweli; basi, watu hao wawili wakatundikwa juu ya muti. Habari juu ya tukio hilo iliandikwa katika kitabu cha Mambo ya Siku mbele ya mufalme.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.