1Maneno haya ni ya Muhubiri mwana wa Daudi, aliyekuwa mufalme kule Yerusalema.
2Muhubiri anasema hivi:
Bure, bure kabisa.
Vyote ni bure!
3Mwanadamu anafaidia nini
kwa jasho lake lote hapa chini ya jua?
4Kizazi kimoja kinapita na kingine kinakuja,
lakini dunia inadumu milele.
5Jua linachomoza na kutua;
linarudi haraka kwa pahali linapotokea.
6Upepo unavuma tokea kusini,
unazunguka mpaka kaskazini.
Unazungukazunguka katika mwendo wake,
kisha unarudia tena katika muzunguko wake siku zote.
7Mito yote inatiririkia ndani ya bahari,
lakini bahari haijai hata kidogo;
kule ambako mito inatiririkia
ndiko kule inaendelea kwenda.
8Mambo yote yanasababisha muchoko,
muchoko mukubwa usioelezeka.
Jicho halichoki kuona,
wala sikio kusikia.
9Yaliyokuwa ndiyo yatakayokuwa,
yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka.
Chini ya jua hakuna jambo jipya.
10Watu wanasema: “Angalia jambo hili ni jipya”,
kumbe limekwisha kutendeka zamani za kale.
11Hakuna mutu anayekumbuka mambo ya zamani,
wala atakayekumbuka yatakayotukia kisha.
Ujuzi wa Muhubiri12Mimi Muhubiri, nilikuwa mufalme wa Israeli, kule Yerusalema.
13Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.
14Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!
15Kitu kilichokunjama hakiwezi kunyooshwa.
Kitu kisichokuwa hakiwezi kuhesabiwa.
16Basi, nikafikiri nikisema: “Nimejipatia hekima nyingi zaidi kupita wote waliopata kutawala Yerusalema mbele yangu. Kweli, ninajua hekima na maarifa ni nini.”
17Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.
18Maana katika kuwa na hekima nyingi kuna wasiwasi;
na anayeongeza maarifa zaidi anaongeza huzuni zaidi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.