1Basi tuseme nini juu ya babu yetu Abrahamu? Nini iliyomutokea?
2Ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo yake, angeweza kujivuna. Lakini hawezi kujivuna mbele ya Mungu.
3Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.”
4Mutu anayefanya kazi, mushahara wake hauhesabiwi kama zawadi, lakini ni haki yake.
5Lakini mutu asipotegemea matendo yake mwenyewe, naye akimwamini Mungu anayemuhesabia mwovu haki, basi imani yake inahesabiwa kuwa haki.
6Na ni vile Daudi anavyosema juu ya uheri wa mutu ambaye Mungu anayehesabia haki pasipo kuangalia matendo yake.
7“Heri wale waliosamehewa makosa yao,
nazo zambi zao zimefutwa.
8Heri mutu yule Bwana asiyemuhesabia zambi zake.”
9Uheri huu si kwa watu wanaotahiriwa tu, lakini ni kwa watu wasiotahiriwa vilevile. Kwa maana tumekwisha kusema kwamba Abrahamu alihesabiwa kuwa mwenye haki kwa njia ya imani yake.
10Yeye alihesabiwa vile alipokuwa katika hali gani? Alipokuwa amekwisha kutahiriwa au alipokuwa hajatahiriwa bado? Halikutendeka nyuma ya kutahiriwa kwa Abrahamu lakini mbele ya kutahiriwa kwake!
11Nyuma ya pale alitahiriwa, na kutahiriwa kwake kulikuwa kitambulisho cha kuhakikisha ile haki Mungu aliyomuhesabia kwa njia ya imani yake. Hivi Abrahamu akakuwa baba wa watu wote wanaoamini, ijapokuwa hawatahiriwi, kusudi wao vilevile wahesabiwe haki.
12Vilevile yeye ni baba ya wale wanaotahiriwa, si kwa sababu wametahiriwa tu, lakini kwa sababu wanafuata vilevile njia ile ile ya imani ambayo babu yetu Abrahamu alifuata alipokuwa hajatahiriwa.
Mungu anatimiza ahadi yake kwa wenye kumutumainia13Mungu alimwahidi Abrahamu na wazao wake kwamba atawapa dunia kuwa urizi wao, si kwa sababu alishika Sheria lakini kwa sababu Mungu alimuhesabia haki kwa njia ya imani yake.
14Kwa maana ikiwa wale wanaotii Sheria ndio watakaopokea kitu anachoahidi, basi imani haina mafaa yoyote, nayo ahadi ya Mungu ni bure.
15Kwa sababu Sheria inaamusha kasirani ya Mungu. Lakini Sheria haingekuwa, kuvunja Sheria hakungekuwa vilevile.
16Kwa hiyo ahadi inafuatana na imani, kusudi ikuwe imetolewa kwa neema ya Mungu. Na zaidi kuwe uhakikisho kwamba ahadi hiyo ni kwa ajili ya wazao wote wa Abrahamu, si kwa wale wanaotii Sheria tu, lakini vilevile kwa wale wanaokuwa na imani kama Abrahamu, babu yetu sisi wote.
17Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Nimekuweka kuwa babu wa mataifa mengi.” Abrahamu alimwamini Mungu, kwa hiyo yeye ni baba yetu mbele yake. Ni yeye Mungu anayewafufua wafu na kuamuru vitu visivyokuwa vipate kuwa.
18Abrahamu aliamini na kutumainia mambo ambayo yasingewezekana kutumainia na hivi akakuwa babu ya mataifa mengi, kufuatana na maneno haya Mungu aliyomwambia: “Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi.”
19Yeye alikuwa na umri wa miaka karibu mia moja, lakini imani yake haikupunguka alipofikiri juu ya hali yake iliyokuwa kama ya mwenye kungojea tu lufu wala juu ya hali ya Sara aliyekuwa hawezi tena kuzaa.
20Hakuona shaka juu ya ahadi aliyopewa na Mungu wala kupoteza tumaini, lakini imani yake ilimutia nguvu hata akamutukuza Mungu.
21Alifanya vile kwa sababu alijua hakika kwamba yule aliyetoa ahadi ile yuko na uwezo wa kuitimiza.
22Kwa sababu hiyo “alihesabiwa kuwa mwenye haki”.
23Lakini maneno hayo “alihesabiwa kuwa mwenye haki” hayakuandikwa kwa ajili yake yeye mwenyewe,
24lakini vilevile kwa ajili yetu sisi tutakaohesabiwa haki. Ndio sisi tunaomwamini yule aliyemufufua Yesu Bwana wetu.
25Alitolewa kufa sababu ya makosa yetu na kufufuliwa kusudi tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.