1Usiwaonee wivu watu waovu,
wala usitamani kuwa pamoja nao,
2maana mafikiri yao yote ni juu ya kutesa tu,
nayo midomo yao inasema mabaya.
3Nyumba inajengwa kwa hekima,
na kuimarishwa kwa ufahamu.
4Kwa maarifa vyumba vyake vinajazwa
vitu vya bei kali na vya kupendeza.
5Kuwa na hekima na maarifa
ni bora kuliko kuwa na nguvu.
6Maana kwa mipango mizuri unaweza kupigana vita,
na kwa washauri wengi ushindi unapatikana.
7Kwa mupumbafu hekima ni ngumu kuielewa;
penye mukutano wa mashauri hafungui mudomo.
8Anayefikiria kutenda maovu siku zote,
ataitwa mutu mwenye fitina.
9Mupango mupambafu anaofikiri ni zambi;
mwenye kuzarau anachukiwa na kila mutu.
10Ukiregea wakati wa shida,
basi wewe ni muzaifu kweli.
11Umwokoe mutu anayepelekwa kuuawa kwa bure;
usisite kumwopoa anayeuawa bila kosa.
12Usiseme kisha: “Hatukujua!”
Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona;
yeye atakulipa kulingana na matendo yako!
13Mwana wangu, ukule asali maana ni nzuri;
sega la asali ni tamu katika kinywa chako.
14Ndivyo hekima itakavyokuwa katika nafsi yako;
ukiipata, siku nzuri zitakuja
na tumaini lako halitakuwa la bure.
15Usivizie kama mwovu kwa kushambulia makao ya mutu wa haki,
wala usijaribu kuharibu nyumba yake,
16maana mutu wa haki anaanguka mara nyingi naye anainuka tena,
lakini mutu mwovu anaangamizwa na hasara.
17Usishangilie kuanguka kwa adui yako;
usifurahie ndani ya moyo wako kujikwaa kwake,
18maana Yawe akiona yale hatapendezwa;
ataacha kumuazibu.
19Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya,
wala usiwaonee wivu watu waovu,
20maana siku mbaya zitamufikia mwovu;
taa ya uzima wake itazimika.
21Mwana wangu, uwaheshimu Yawe na mufalme,
wala usishirikiane na waasi,
22maana maangamizi yatawatokea kwa rafla.
Hakuna anayejua magumu watakayoleta.
Misemo zaidi23Hii ni misemo mingine ya wenye hekima.
Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.
24Anayemwachilia mutu mwenye kosa analaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa.
25Lakini wanaowaazibu waovu watapata furaha, na baraka nzuri zitawafikia.
26Jibu linalokuwa la haki ni kama busu la rafiki.
27Kwanza fanya kazi zako inje na kutayarisha kila kitu katika shamba. Kisha jenga nyumba yako.
28Usishuhudie bure juu ya jirani yako, wala usiseme uongo juu yake.
29Usiseme: “Nitamutendea kama vile alivyonitendea! Inapasa kulipiza kisasi!”
30Nilipitia karibu na shamba la muvivu, ni kusema shamba la mizabibu la mutu mupumbafu,
31niliona kwamba lilikuwa limeota miiba, majani yalikuwa yamefunika eneo lake lote, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32Niliangalia, nikawaza. Kwa mwisho nikapata fundisho:
33Lala tu kidogo,
sinzia tu kidogo,
kunja mikono yako tu upumzike,
34lakini kumbuka kwamba
unapokuwa katika usingizi,
umasikini utakufikia kama munyanganyi,
ukosefu kama mutu mwenye silaha.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.