1Haya ndiyo maneno nabii Yeremia aliyosema katika mwaka wa ine wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda na Baruku mwana wa Neria akayaandika katika kitabu:
2Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu yako wewe Baruku:
3Wewe ulisema: Ole wangu! Yawe ameongezea uchungu juu ya maumivu yangu. Nimechoka na kulalamika, wala siwezi kupumzika.
4Lakini Yawe ameniambia nikuambie:
Yawe anasema hivi: Yale niliyojenga ninayabomoa, na yale niliyopanda ninayaongoa; nitafanya hivyo katika inchi yote.
5Wewe unajitakia wewe mwenyewe mambo makubwamakubwa? Usiyatafute! Achana nayo, maana ninaleta maangamizi juu ya wanadamu wote. Pato lako ni hili: nitayaokoa maisha yako kila nafasi utakapokwenda.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.