1Zaburi ya Daudi: Mashairi.
Heri mutu aliyesamehewa kosa lake,
mutu ambaye zambi yake imeondolewa kabisa.
2Heri mutu ambaye Yawe hamuhesabii kosa,
mutu ambaye hana udanganyifu ndani ya moyo wake.
3Nilipokuwa sijaitikia zambi yangu,
nilikuwa muzaifu sana kwa kulia muchana kutwa.
4Muchana na usiku mukono wako ulinilemea;
nguvu zangu zikakwisha,
kama maji yanavyokauka wakati wa kipwa.
5Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako,
wala sikuficha uovu wangu.
Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe.
Nawe ukanisamehe zambi yangu.
6Kwa hiyo, kila mwaminifu akutolee maombi
wakati wa taabu.
Mafuriko ya maji hayatamufikia.
7Wewe unanificha
kwa kunilinda wakati wa taabu.
Ninazungukwa na ukombozi wako.
8Mungu anasema: “Nitakufundisha
na kukuonyesha njia utakayofuata.
Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.
9Usikuwe mupumbafu kama farasi au nyumbu,
ambao lazima wafungwe kamba ndani ya kinywa,
kama sivyo hawatakukaribia.”
10Watu waovu watapata mateso mengi,
lakini wanaomutumainia Yawe
wanazungukwa na wema wake.
11Mufurahi na kushangilia kwa sababu ya Yawe,
enyi watu wa haki;
mupige vigelegele vya shangwe, enyi wenye moyo wa usawa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.