1Yesu alipomaliza kutoa maagizo hayo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, akaondoka kule, akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji ya inchi ile.
2Yoane Mubatizaji, akiwa katika kifungo, akapata habari za mambo Kristo aliyokuwa akifanya. Basi akawatuma wanafunzi wake
3kumwuliza Yesu: “Wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja kutuokoa au tumungojee mwingine?”
4Yesu akawajibu: “Mwende kumwelezea Yoane mambo munayosikia na kuyaona:
5vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.
6Heri mutu yule mimi sitakayekuwa kikwazo kwake!”
7Wale wanafunzi wa Yoane walipoondoka, Yesu akaanza kuwaambia makundi ya watu habari za Yoane: “Mulienda katika jangwa kwa kuangalia nini? Tete linalotikiswa na upepo? Hapana!
8Basi mulienda kuona nini? Mutu aliyevaa nguo nzuri? Hapana! Wale wanaovaa nguo nzuri wanakaa katika nyumba za wafalme.
9Basi mulikwenda kuona nini? Nabii? Ndiyo, ninawaambia, yeye ni mukubwa kupita hata nabii.
10Huyu ndiye maneno haya yameandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu: ‘Ninamutuma mujumbe wangu akutangulie, kusudi akutengenezee njia utakayopitia!’
11“Kweli ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna mutu anayekuwa mukubwa kuliko Yoane Mubatizaji. Lakini yeyote anayeonekana kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.
12Tangia wakati Yoane Mubatizaji alipohubiri mpaka sasa, watu wanapinga Ufalme wa mbinguni, nao watu wakali wanajaribu kuukamata kwa kinguvu.
13Kwa maana mambo hayo yalitangazwa na manabii wote na Sheria ya Musa mpaka wakati wa Yoane.
14Na ikiwa munasadiki, Yoane ndiye nabii Elia aliyepaswa kuja.
15Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!
16“Nitawafananisha watu wa kizazi hiki na nini? Wanafanana na watoto wanaoikaa kwenye nafasi ya makutano na kuita wenzao wakisema:
17‘Tuliwapigia ngoma, lakini hamukucheza! Tuliimba wimbo wa kilio, lakini hamukulia!’
18Kwa maana Yoane alikuja, alifunga kula chakula na kunywa, nao wakasema: ‘Yuko na pepo!’
19Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”
Azabu ya miji iliyokataa kumwamini Yesu(Lk 10.13-15)20Kisha Yesu akaanza kuonya miji ambamo alifanya miujiza mingi zaidi, kwa sababu wakaaji wa kule hawakugeuka toka zambi zao. Akasema:
21“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.
22Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, ninyi mutaazibiwa zaidi kuliko muji wa Tiro na wa Sidona.
23Nawe, muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka juu mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu. Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yako ingalifanyika katika Sodoma, muji ule ungekuwa ungali hata leo.
24Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, wewe utaazibiwa zaidi kuliko watu wa Sodoma!”
Yesu anamushukuru Mungu(Lk 10.21-22)25Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.
26Ndiyo, Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.
27“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.
Maonyo kwa wenye kusumbuka28“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.
29Mukubali kuongozwa nami kama vile ngombe dume anayefungiwa nira, nanyi mufuate mafundisho yangu maana mimi ni mupole na munyenyekevu. Kwa hiyo mutapumzika.
30Nira yangu si nzito, nao muzigo nitakaowabebesha ni mwepesi.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.