1Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”
2Kisha, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi:
3“Ondoka hapa uelekee upande wa mashariki, ujifiche kwenye kijito cha Keriti kinachokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.
4Kule, utapata maji ya kunywa katika kijito kile. Tena nimewaamuru vibombobombo wakuletee chakula.”
5Basi, Elia akatii agizo la Yawe, akaenda kukaa kwenye kijito cha Keriti kinachokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.
6Vibombobombo wakakuwa wanamuletea mukate na nyama, asubui na magaribi; akapata na maji ya kunywa katika kijito kile.
7Lakini, nyuma ya siku chache kijito kikakauka kwa sababu hakukunyesha mvua katika inchi.
Elia na mujane wa Zerepata8Hapo, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi:
9“Ondoka uende katika muji wa Zerepata, karibu na Sidona, ukae kule. Nimemwamuru mujane mumoja akupatie chakula kule.”
10Basi, Elia akaondoka, akaenda Zerepata. Alipofika kwenye mulango wa muji, akamukuta mwanamuke mumoja mujane akiokota kuni. Elia akamwita mwanamuke huyo na kumwambia: “Uniletee maji nikunywe.”
11Yule mwanamuke alipokuwa anaondoka, Elia akamwita tena na kumwambia: “Uniletee na kipande cha mukate vilevile.”
12Huyo mwanamuke akamwambia: “Kama vile Yawe Mungu wako anavyoishi, sina mukate hata kidogo. Niko tu na unga unaoweza kujaa mukono mumoja katika chungu na mafuta kidogo katika chupa. Nimefika hapa kuokota kuni, kisha niende kwangu kupika chakula hicho, mwana wangu na mimi tukule, kisha tungojee kufa.”
13Elia akamwambia: “Usiogope. Kwenda ufanye kama vile ulivyosema. Lakini unitengenezee mimi kwanza na kuniletea andazi dogo, kisha ujitengenezee wewe na mwana wako chakula.
14Maana, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Unga unaokuwa ndani ya chungu chako hautapunguka wala mafuta yanayokuwa ndani ya chupa hayatakwisha, mpaka pale mimi Yawe nitakaponyesha mvua katika inchi.’ ”
15Basi, yule mwanamuke mujane akaenda akafanya kama vile alivyoambiwa na Elia hata mama huyo, jamaa yake na Elia wakapata chakula kwa siku nyingi.
16Unga ndani ya chungu haukupunguka, wala mafuta katika chupa hayakuisha sawa kabisa na neno la Yawe alilomwambia Elia aseme.
Elia anamufufua mutoto wa mama mujane17Nyuma ya hayo, mwana wa mwanamuke huyo mwenye nyumba akagonjwa, na hali yake ikazidi kuwa mbaya, hata kwa mwisho akakufa.
18Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”
19Elia akamwambia: “Unipe mwana wako.” Basi, Elia akamutwaa mutoto toka kifua cha mama yake, akamupeleka juu katika chumba chake, akamulalisha juu ya kitanda chake.
20Kisha akamusihi Yawe akisema: “Ee Yawe, Mungu wangu, hata mwanamuke huyu mujane ambaye ninakaa kwake, naye ananitunza, unamuletea hasara kwa kumwua mwana wake?”
21Kisha Elia akajinyoosha juu ya mutoto yule mara tatu na kumwomba Yawe: “Ee Yawe, Mungu wangu, umurudishie mutoto huyu roho yake!”
22Yawe akasikiliza ombi la Elia. Mutoto akaanza kupumua tena.
23Elia akamurudisha mutoto chini kwa mama yake, akamwambia: “Angalia! Mwana wako yuko muzima.”
24Huyo mwanamuke mujane akamwambia Elia: “Sasa ninajua kwa hakika kwamba wewe ni mutu wa Mungu, na maneno Yawe aliyokupa uyaseme ni ya kweli.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.