Kutoka 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maagizo juu ya malipo

1Mwizi akikamatwa yuko anavunja nyumba, naye akipigwa na kufa, aliyemwua hana kosa la mauaji.

2Lakini mwizi akishikwa wakati jua limechomoza na kuuawa, aliyemwua atakuwa na kosa.

Mwizi anapaswa kulipa. Ikiwa hana kitu cha kulipa, basi, yeye mwenyewe atauzishwa kwa kulipa kile alichoiba.

3Kama nyama aliyeibwa, akuwe ni ngombe, punda au kondoo, akipatikana muzima kwa mwizi, basi, yule mwizi atalipa nyama wawili.

4Mutu akiwakulishia nyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachilia nyama wake kula katika shamba la mutu mwingine, atalipa hasara ile kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.

5Mutu akiwasha moto nao ukichoma miti ya miiba na kusambaa mpaka kuteketeza miganda ya ngano au ngano ya mutu mwingine ambayo bado haijavunwa au shamba lote likiteketea, aliyewasha moto ule anapaswa kulipa hasara ile yote.

6Mutu akimwachia mwenzake feza au mali nyingine amutunzie, kisha ikaibiwa ndani ya nyumba yake, mwizi akipatikana anapaswa kulipa bei yake mara mbili.

7Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atakaribia mbele ya Mungu kwa kuhakikisha kwamba yeye hakuiba mali ya mwenzake.

8Kukitokea ubishi juu ya ngombe, au punda, au kondoo, au nguo, au kitu chochote kilichopotea ambacho kila mumoja anadai kwamba ni chake, wale wanaobishana wataletwa mbele ya Mungu. Yule ambaye Mungu ataamua kwamba amekosa, atamulipa mwenzake mara mbili.

9Mutu akimupatia mwenzake punda, ngombe, kondoo au nyama mwingine yeyote amutunzie na nyama yule akikufa au akipelekwa bila mutu yeyote kushuhudia,

10kiapo mbele ya Yawe kitaamua kati yao, kwa kuonyesha kwamba yule aliyepewa hakuiba mali ya mwenzake. Mwenye nyama yule atakubali kile kiapo na yule mwenzake hatalipa malipo yoyote.

11Lakini kama aliibiwa kwake, anapaswa kumulipa mwenye naye.

12Kama yule nyama aliraruliwa na nyama wa pori, yule mutu aliyekuwa amepewa anapaswa kumuleta kama ushuhuda. Hatalipa malipo yoyote kwa ajili ya nyama aliyeraruliwa na nyama wa pori.

13Mutu akiazima nyama kwa mwenzake, kisha nyama yule akaumia au akakufa wakati mwenye naye hayuko, aliyeazima nyama yule anapaswa kumulipa kwa ukamilifu.

14Lakini kama mwenye naye alikuwa pale, basi aliyemwazima hatalipa kitu chochote. Kama alikuwa ni nyama aliyeazimwa, mwenye naye atakubali tu bei ya kuazima.

Sheria za namna ya kuishi

15Mutu akimutongoza binti ambaye hajachumbiwa, akilala naye, hakika atalipa mali na kumwoa binti yule.

28Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.

29Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu.

Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.

30Ninyi mutakuwa watu waliotakaswa kwa ajili yangu. Kwa hiyo hamutakula nyama ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori. Nyama hiyo mutaitupia imbwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help