Zaburi 55 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maombi ya mutu anayeteswa

1Kutoka kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Mashairi ya Daudi.

2Ee Mungu, tega sikio usikie maombi yangu;

usiangalie pembeni ninapokuomba.

3Unisikilize na kunijibu;

nimechoka na malalamiko yangu.

4Nina hofu kwa ajili ya vitisho vya waadui zangu,

na kwa kuteswa na watu waovu.

Watu waovu wananitaabisha,

kwa hasira wananishambulia.

5Moyo wangu umejaa hofu,

vitisho vya kifo vimenisonga.

6Ninatetemeka kwa hofu kubwa,

nimeshikwa na vitisho vikubwa.

7Ninasema hivi: “Heri ningekuwa na mabawa kama njiwa!

Ningeruka mbali na kupata pumziko,

8ningesafiri mbali sana,

ningepata makao katika jangwa,

9ningekimbilia pahali penye usalama,

mbali na upepo mukali na zoruba.”

10Ee Bwana, uwaangamize na kuvuruga luga yao,

maana ninaona mateso ya ukali na ugomvi katika muji,

11vikiuzunguka muchana na usiku,

na kuujaza hasara na ukorofi.

12Uharibifu umeenea popote katika muji,

maovu na mapotovu kila pahali.

13Kama adui yangu angenitukana,

ningeweza kuvumilia hayo;

kama mupinzani wangu angenizarau,

ningeweza kujificha mbali naye.

14Lakini, kumbe ni wewe mwenzangu;

ni wewe rafiki yangu wa kweli!

15Sisi tulizoea kuzungumuza kirafiki;

pamoja tulikwenda katika nyumba ya Mungu.

16Acha kifo kiwashitukie waadui zangu,

washuke chini katika kuzimu wangali wazima;

maana uovu umejaa katika mioyo yao.

17Lakini mimi ninamulilia Mungu,

naye Yawe ataniokoa.

18Magaribi, asubui na muchana kati, ninalalamika na kulia,

naye atasikia sauti yangu.

19Atanikomboa katika vita na kunipa amani,

kwa maana waadui zangu ni wengi.

20Mungu anayetawala tangu milele,

atanisikia na kuwafezehesha waadui yangu,

maana hawapendi kubadilika,

wala hawamwogopi Mungu.

21Mwenzangu amemushambulia rafiki yake,

amevunja mapatano yake.

22Maneno yake ni matamu kuliko maziwa,

lakini mawazo yake ni ya kufanya vita.

Maneno yake ni laini kama mafuta,

lakini yanakata kama upanga mukali.

23Utue muzigo wako kwa Yawe,

naye atakusaidia;

hamwachilii mutu wa haki ashindwe.

24Wewe, ee Mungu, utawaporomosha katika shimo chini kabisa.

Wauaji na wadanganyifu hawatafikia nusu ya maisha yao.

Lakini mimi nitakutumainia wewe, ee Mungu!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help