1Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.
2Yeye alikuwa mwaminifu mbele ya Mungu aliyemusimika kwa kazi ile, sawa vile Musa alivyokuwa mutumishi mwaminifu katika kazi ya nyumba yote ya Mungu.
3Mujengaji wa nyumba anaheshimiwa zaidi kuliko nyumba yenyewe. Hivi vilevile Yesu anastahili kupewa heshima kubwa zaidi kuliko Musa.
4Ni kweli kila nyumba inajengwa na mutu, lakini Mungu ndiye aliyejenga vitu vyote.
5Musa alikuwa mutumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, kusudi ashuhudie maneno ambayo Mungu angesema nyuma.
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.
Mapumziko Mungu anayotayarishia watu wake7Kwa hiyo, kama vile Roho Mutakatifu anavyosema:
“Leo ikiwa munasikiliza sauti ya Mungu,
8musifanye mioyo yenu kuwa migumu
kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu,
sawa siku ile walipomupima katika jangwa.
9Kule babu zenu walinipima na kunijaribia,
ingawa walikuwa wameona yote niliyotenda kwa muda wa miaka makumi ine.
10Kwa sababu ile nilikasirikia kizazi chao,
na kusema: Watu hao wanapotoka siku zote.
Nao hawafuati njia zangu.
11Basi nikaapa kwa kasirani
kwamba hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia!”
12Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.
13Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.
14Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.
15Maandiko Matakatifu yanasema:
“Leo ikiwa munasikiliza sauti ya Mungu,
musifanye mioyo yenu kuwa migumu
kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu.”
16Ni watu gani waliosikia maneno ya Mungu na kumwasi? Si wale wote walioongozwa na Musa toka katika inchi ya Misri?
17Tena, ni watu gani waliomukasirikisha Mungu kwa muda wa miaka makumi ine? Si wale wote waliofanya zambi wakaanguka na kufa katika jangwa?
18Tena ni watu gani Mungu aliowaapia kwamba hawataingia kwenye mapumziko aliyowatayarishia? Si wale waliokataa kumutii?
19Basi tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwenye mapumziko yale kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.