1Wandugu zangu, ninataka mukumbuke kwamba babu zetu wote walisafiri wakiongozwa na wingu, nao wote walivuka katikati ya bahari Nyekundu kwa usalama.
2Wote walibatizwa katika lile wingu na katika ile bahari kusudi wapate kuungana na Musa.
3Wote walikula chakula kimoja cha kiroho.
4Wote walikunywa kinywaji kimoja cha kiroho; kwa maana walikunywa maji yaliyotoka ndani ya lile jiwe lililosafiri pamoja nao, nalo jiwe lilikuwa Kristo.
5Lakini, wengi sana kati yao hawakumupendeza Mungu, kwa hiyo wakakufia katika jangwa.
6Mambo hayo ni mufano kwetu, kusudi tusikuwe na tamaa mbaya kama vile wao.
7Basi musikuwe wenye kuabudu sanamu kama wamoja kati yao walivyokuwa; kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema: “Watu wakaikaa kula na kunywa na kisha wakasimama kwa kujifurahisha.”
8Musifanye uasherati kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata wakakufa kwa siku moja watu elfu makumi mbili na tatu.
9Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.
10Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.
11Mambo haya yote yaliwafikia kusudi yakuwe mufano kwa watu wengine; yameandikwa kwa kutuonya sisi, kwa maana tunaishi katika kipindi cha mwisho wa nyakati.
12Kwa hiyo yule anayefikiri kwamba anasimama imara, afanye angalisho asianguke.
13Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.
14Kwa hiyo wapenzi wangu, muepuke kutambikia sanamu.
15Ninasema nanyi kama watu wenye akili; muamue ninyi wenyewe juu ya maneno ninayotaka kuwaambia:
16tunapokunywa kikombe ambacho kwa ajili yake tunamutolea Mungu shukrani, basi kwa njia ya kikombe kile hatuungani na damu ya Kristo? Nasi tunapomega mukate na kuukula, kwa njia hiyo, mukate ule hautuungi na mwili wa Kristo?
17Kwa kuwa mukate ni mumoja, ijapokuwa sisi ni wengi, tuko mwili mumoja, kwa maana sisi wote tunashiriki mukate ule mumoja.
18Muangalie mufano wa Waisraeli: wale wanaokula vitu vinavyotolewa sadaka juu ya mazabahu wanaungana na Mungu kwa njia ya sadaka ile.
19Basi niseme nini? Nyama iliyotambikiwa kwa sanamu ni yenye mafaa? Au kwamba sanamu ni kitu cha lazima?
20Hapana. Ninataka kusema kwamba vitu wapagani wanavyotambikia, wanavitolea pepo wala si Mungu. Nami sipendi mushirikiane na pepo hata mara moja.
21Hamuwezi kuchangia kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo. Vilevile hamuwezi kuchangia meza ya Bwana na meza ya pepo.
22Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?
Kufanya yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu23Wamoja wenu wanasema: “Vitu vyote vinaruhusiwa.” Ni kweli, lakini vyote havifai. “Vitu vyote vinaruhusiwa,” lakini vyote havifai kwa kujenga imani.
24Mutu asitafute faida yake mwenyewe, lakini faida ya mwenzake.
25Ninyi ni huru kwa kula kila kitu kinachouzishwa katika soko bila kuulizauliza neno kwa sababu ya zamiri.
26Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Bwana.”
27Kama mupagani anawaalika kula chakula, nanyi mukikubali kwenda kule, mukule vyote wanavyotoa kwenu bila kuulizauliza neno kwa sababu ya zamiri.
28Lakini kama mutu akiwaambia ninyi: “Vyakula hivi vimetambikiwa kwa sanamu,” basi musivikule kwa ajili ya yule aliyewaarifu na kwa ajili ya zamiri.
29Sisemi juu ya zamiri zenu, lakini juu ya zamiri ya yule aliyewaarifu.
Labda kuna mutu anayeweza kuuliza: “Kwa sababu gani ninaweza kuzuizwa kutenda sawa na uhuru wangu kwa ajili ya mwingine?
30Kama ninamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula ninachokula, kwa nini wananiteta juu ya chakula ambacho kwa ajili yake ninamutolea Mungu shukrani?”
31Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
32Basi muangalie, kusudi musiwakwaze Wayuda, wala wasiokuwa Wayuda, wala kanisa la Mungu.
33Mufanye kama vile mimi: ninajikaza kwa kupendeza watu wote katika mambo yote, maana sitafuti faida yangu mimi mwenyewe, lakini faida ya watu wote, kusudi waokolewe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.