1Yawe anasema hivi:
Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki,
maana ninakaribia kuwaokoa,
watu wataona wazi kwamba ninawakomboa.
2Heri mutu anayefuata maneno hayo,
anayeshika kabisa siku za Sabato kwa heshima
na kuepuka kutenda uovu wowote.
3Mugeni anayenitambua mimi Yawe asifikiri hivi:
Hakika Yawe atanitenga na watu wake.
Naye towashi asiseme:
Mimi ni muti wenye kukauka!
4Maana Yawe anasema hivi:
Towashi anayeshika siku zangu za Sabato,
anayefanya mambo yanayonipendeza,
na kuchunga agano langu,
5nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa
katika nyumba yangu na kuta zangu,
nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti.
Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote
na ambalo halitafutwa hata kidogo.
6Wageni watakaoshikamana nami Yawe,
kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu,
na kuwa watumishi wangu,
wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua,
watu watakaofuata agano langu,
7hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu,
na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi;
sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu.
Maana nyumba yangu itaitwa:
Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.
8–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.–
Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya,
nitawakusanya watu wengine wakutane nao.
Wasimamizi wa Waisraeli wanashitakiwa9Enyi nyama wote wakali,
nanyi nyama wote wa pori,
mukuje mukule.
10Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu;
wote hawana akili yoyote.
Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka,
wanalala tu na kuota ndoto,
wanapenda sana kusinzia!
11Hao ni kama imbwa walafi sana,
wala hawawezi kutosheka hata kidogo.
Wachungaji nao hawana akili yoyote.
Kila mumoja anatafuta njia yake mwenyewe,
kila mumoja anatafuta faida yake.
12Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai;
mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali!
Kesho itakuwa kama leo,
tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.