1 Wafalme 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Siku za mwisho za mufalme Daudi

1Wakati mufalme Daudi alipokuwa muzee sana, watumishi wake walimufunika kwa mablanketi, lakini, hata hivyo, hakuweza kupata joto.

2Kwa hivyo, wakamwambia: “Bwana wetu mufalme, afazali tukutafutie binti akutumikie na kukutunza; alale pamoja nawe kusudi akupatie joto.”

3Basi, wakatafutatafuta binti muzuri katika inchi yote ya Israeli. Kukapatikana binti mumoja muzuri anayeitwa Abisagi Musunami. Wakamuleta kwa mufalme.

4Binti yule, alikuwa muzuri sana. Basi, akaanza kumutumikia na kumutunza mufalme, lakini mufalme hakumujua kimwili.

Adonia anajitafutia ufalme

5Wakati ule, Adonia mwana wa Daudi kutoka muke wake Hagiti, akaanza kujivuna kwamba yeye ndiye atakayekuwa mufalme. Basi, akajitayarishia magari, wapanda-farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.

6Lakini baba yake Daudi hakukuwa amemukaripia mwana wake hata mara moja wala kumwuliza kwa nini alikuwa amefanya hivyo. Adonia alikuwa mwenye sura ya kupendeza sana na alikuwa amemufuata Abusaloma kwa kuzaliwa.

7Adonia akafanya shauri na Yoabu mwana wa Zeruya, na kuhani Abiatari. Nao wakamufuata na kumwunga mukono.

8Lakini kuhani Zadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Natani na Simei, na Rei pamoja na walinzi wa Daudi, hawakumwunga Adonia mukono.

9Siku moja, Adonia alitoa sadaka ya kondoo, ngombe na wana-ngombe wanono kwenye Jiwe la Zoheleti, karibu na chemichemi inayoitwa Enrogeli. Akawaalika kwenye karamu ya sadaka hiyo wandugu zake wote, ni kusema wana wengine wa mufalme, na watumishi wote wa mufalme wanaokuwa wa kabila la Yuda.

10Lakini hakuwaalika nabii Natani, Benaya, walinzi wa mufalme na ndugu yake Solomono.

Solomono anawekwa kuwa mufalme

11Kisha, Natani akamwendea Batiseba mama ya Solomono, akamwuliza: “Haujasikia kwamba Adonia mwana wa Hagiti amejiweka kuwa mufalme na bwana wetu Daudi hana habari?

12Basi, kama ukitaka kuyaokoa maisha yako na ya mwana wako Solomono, ninakushauria hivi:

13Umwendee mufalme Daudi, umwulize: ‘Bwana wangu mufalme, si uliniapia mimi mujakazi wako ukisema: Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme? Imekuwa namna gani basi, sasa Adonia anatawala?’

14Na utakapokuwa ungali unaongea na mufalme, mimi nitaingia na kuyahakikisha maneno yako.”

15Basi, Batiseba alimwendea mufalme ndani ya chumba chake. Wakati ule, mufalme alikuwa muzee sana, naye Abisagi Musunami alikuwa akimuchunga.

16Batiseba aliinama kwa heshima mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: “Unataka nini?”

17Batiseba akamujibu: “Bwana wangu, uliniapia mimi mujakazi wako mbele ya Mungu wako Yawe, ukisema: ‘Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme.’

18Lakini, sasa, Adonia anatawala ingawa wewe bwana wangu mufalme haujui juu ya hayo.

19Ametoa sadaka ya ngombe, ya wana-ngombe wanono, na kondoo wengi, na amewaalika wana wote wa mufalme, kuhani Abiatari, na Yoabu jemadari wa makundi yako ya waaskari, lakini mutumishi wako Solomono hakualikwa.

20Na sasa, bwana wangu mufalme, Waisraeli wote wanakungojea, kusudi uwaambie yule atakayeikaa juu ya kiti chako nyuma yako, bwana wangu mufalme.

21Na kama sivyo, itatokea kwamba, wakati wewe bwana wangu mufalme utakapokufa, mimi pamoja na mwana wangu Solomono tutahesabiwa kama wenye kosa.”

22Wakati Batiseba alipokuwa akizungumuza na mufalme, nabii Natani aliingia katika nyumba ya kifalme.

23Nao watu wakamwambia mufalme: “Nabii Natani yuko hapa.” Naye alipomufikia mufalme, aliinama mbele ya mufalme mpaka uso ukafika chini kwenye udongo.

24Halafu Natani akasema: “Bwana wangu mufalme, ni kweli kwamba ulisema hivi: ‘Adonia atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme’?

25Kwa maana leo alienda kutoa sadaka ya ngombe, wana-ngombe wanono na kondoo wengi na amewaalika wana wote wa mufalme, Yoabu jemadari wa waaskari, na kuhani Abiatari, na sasa wanakula na kunywa mbele yake, na kusema: ‘Mufalme Adonia aishi!’

26Lakini hakunialika mimi mutumishi wako wala kuhani Zadoki wala Benaya mwana wa Yehoyada wala mutumishi wako Solomono.

27Mbona yote hayo umeyafanya wewe bwana wangu mufalme, bila kuwaambia watumishi wako mutu atakayeikaa juu ya kiti chako cha kifalme nyuma yako?”

28Naye mufalme Daudi akajibu: “Uniitie Batiseba.” Batiseba alimwendea mufalme na kusimama mbele yake.

29Halafu mufalme aliapa, akisema: “Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyekomboa roho yangu katika taabu nyingi,

30kama nilivyokuapia mbele ya Yawe, Mungu wa Israeli, nikisema: ‘Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme pahali pangu’, ndivyo nitakavyofanya leo.”

31Batiseba akainama uso mpaka chini, kwa heshima mbele ya mufalme, na kusema: “Bwana wangu mufalme Daudi aishi milele!”

32Kisha mufalme Daudi akasema: “Uniitie kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Nao wakafika kwa mufalme.

33Naye mufalme akawaambia: “Kwenda na watumishi wangu mimi bwana wako, umupandishe mwana wangu Solomono juu ya nyumbu wangu, umupeleke kule Gihoni.

34Halafu umuruhusu kuhani Zadoki na nabii Natani wamupakae mafuta akuwe mufalme wa Israeli. Kisha mupige baragumu na kusema: ‘Mufalme Solomono aishi!’

35Nanyi mutamufuata, naye atakuja na kuikaa juu ya kiti changu cha kifalme kwa pahali pangu; nami nimemuchagua kuwa mutawala juu ya Israeli na juu ya Yuda.”

36Benaya mwana wa Yehoyada akamujibu mufalme: “Amina! Yawe, Mungu wa bwana wangu mufalme, aseme vile vile.

37Kama Yawe alivyokuwa pamoja na bwana wangu mufalme, akuwe vilevile na Solomono, na akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti cha kifalme cha bwana wangu mufalme Daudi.”

38Basi, kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, wote walishuka, wakamupandisha Solomono kwenye nyumbu wa mufalme Daudi, na kumupeleka mpaka Gihoni.

39Kisha kuhani Zadoki alitwaa pembe za mafuta kutoka katika hema na kumupakaa Solomono mafuta kuwa mufalme. Kisha walipiga baragumu na watu wote wakasema: “Mufalme Solomono aishi!”

40Halafu watu wote walimufuata, wakipiga mazomari, wakafurahi kwa shangwe kubwa, hata inchi ikatikisika kwa sauti zao.

41Basi, Adonia pamoja na waalikwa waliokuwa naye walikuwa wakimaliza sherehe. Naye Yoabu aliposikia sauti ya baragumu, alisema: “Makelele hayo katika muji ni ya nini?”

42Alipokuwa akisema, Yonatani mwana wa kuhani Abiatari akaingia. Adonia akasema: “Karibu, maana wewe ni mutu hodari na unaleta habari nzuri.”

43Yonatani akamujibu Adonia: “Hapana. Mufalme Daudi amemusimika Solomono kuwa mufalme.

44Naye mufalme amemupeleka pamoja na kuhani Zadoki, nabii Natani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, nao wamemupandisha juu ya nyumbu wa mufalme.

45Kisha kuhani Zadoki na nabii Natani wakamupakaa mafuta akuwe mufalme kule Gihoni. Halafu wametoka hapo wakifurahi, ndiyo sababu ya makelele hayo unayosikia.

46Sasa Solomono anaikaa juu ya kiti cha kifalme.

47Zaidi ya hayo, watumishi wa mufalme walikuja kumupa pole bwana wetu mufalme Daudi wakisema: ‘Mungu wako alifanye jina la Solomono kuwa lenye sifa kuliko lako; tena akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti chako.’ Halafu mufalme akainama juu ya kitanda

48na kuomba akisema: ‘Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye amemufanya muzao wangu kuwa mufalme kwa pahali pangu, na ambaye amenipa maisha hata nimeyaona mambo hayo.’ ”

49Basi, waalikwa wa Adonia wakaogopa sana, wakaondoka na kutawanyika.

50Naye Adonia, kwa sababu alimwogopa Solomono, akakimbilia katika hema la Yawe, akazishika pembe za mazabahu apate kuponyoka.

51Mufalme Solomono akapata habari kwamba Adonia alikuwa amekimbilia ndani ya hema, na kwamba anashikilia pembe za mazabahu akisema: “Sitaondoka hapa mpaka mufalme Solomono atakaponihakikishia kwamba hataamuru niuawe.”

52Mufalme Solomono akasema: “Nikimwona kuwa mwaminifu basi, hatapata hasara yoyote. Lakini nikimwona kuwa mwovu, hakika atakufa.”

53Basi, mufalme Solomono akaagiza Adonia aitwe kutoka katika hema, akuje kwake. Adonia akafika mbele ya mufalme, akainama kwa heshima. Mufalme akamwambia: “Kwenda kwa nyumba yako.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help