1Lakini Sanibalati, Tobia, Waarabu, Waamoni na Waasidodi waliposikia kwamba ujenzi mupya wa ukuta wa Yerusalema ulikuwa unasonga mbele na kwamba nafasi zilizobomoka katika ukuta zimezibwa, wao walizidi kukasirika.
2Kwa hiyo wakafanya shauri baya kwa kuja pamoja Yerusalema kutushambulia na hivyo kuleta muvurugano katika muji ule.
3Halafu tukamwomba Mungu wetu na kuweka ulinzi juu yao, muchana na usiku.
4Watu wa Yuda wakakuwa wanalalamika wakisema: “Tunachoka na kubeba mizigo na bado kuna takataka nyingi za kubeba. Hatuwezi kuendelea kujenga ukuta.”
5Nao waadui zetu wakakuwa wanasema: “Hawataweza kujua wala kuona, mpaka tutakapokuwa kati yao; tutawaua na kusimamisha kazi.”
6Wayuda waliokaa kati ya waadui zetu waliposikia maneno yao, mara kwa mara, walitufikia mara kumi wakisema: “Watakuja toka kila pahali wanapokaa na kutushambulia.”
7Hivyo, kwenye sehemu za chini za ukuta ambazo zilikuwa bado kumalizika, nyuma ya ukuta, katika pahali pa wazi, nikawapanga watu kulingana na jamaa zao wakiwa na mapanga, mikuki na pinde.
8Nilipoona kwamba watu walikuwa na hofu nikawaambia wakubwa, wasimamizi na watu wote kwa jumla: “Musiwaogope hata kidogo. Mukumbuke Bwana anayekuwa mukubwa na wa kutisha, basi mupigane kwa ajili ya wandugu zenu, wana wenu, wabinti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”
9Waadui waliposikia kwamba tumekwisha kuvumbua mipango yao na kwamba Mungu amevuruga mipango hiyo, ndipo sisi wote tukaurudilia ukuta, kila mumoja akaendelea na kazi yake.
10Tokea siku ile na kuendelea, nusu ya watumishi wangu wakakuwa wanaendelea na ujenzi wakati nusu ingine ikakuwa inashika ulinzi wakiwa na mikuki, ngao, pinde na nguo za chuma. Viongozi wetu wakakuwa upande wa watu wa Yuda
11waliokuwa wanajenga ukuta. Hata wale waliokuwa wanabeba vifaa vya ujenzi wakaendelea na kazi mukono mumoja ukiwa na vifaa vya ujenzi na mukono mwingine silaha yake.
12Kila mujengaji alikuwa na upanga wake ukifungwa kwenye kiuno chake naye akiendelea kujenga. Na mutu wa kupiga baragumu alikuwa karibu nami.
13Nikawaambia wakubwa, wasimamizi na watu wote kwa jumla: “Kazi ni kubwa, na kuna hatua kubwa kati ya mutu na mwenzake juu ya ukuta.
14Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”
15Hivyo, tukaendelea kufanya kazi yetu na nusu ya watu wakishika silaha tangu mapambazuko mpaka nyota zinapoonekana mbinguni.
16Wakati ule nikawaambia watu: “Kila mwanaume na mutumishi wake atakaa katika Yerusalema usiku, kusudi tukuwe na ulinzi usiku, na wakati wa muchana wataendelea na kazi.”
17Hivyo ikakuwa mimi, wandugu zangu, watumishi wangu hata na walinzi waliofuatana nami, hatukuvua nguo zetu; kila mumoja wetu akakuwa na silaha yake katika mukono siku zote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.