Zaburi 137 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maombolezo katika inchi ya kigeni

1kandokando ya mito ya Babeli tuliikaa tukilia,

tulipokumbuka Sayuni.

2Katika miti ya inchi ile,

tulitundika zeze zetu.

3Waliotupeleka kuwa watumwa walitaka tuwaimbie;

watesaji wetu walitaka tuwafurahishe, wakituambia:

“Mutuimbie nyimbo zimoja za Sayuni!”

4Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa Yawe

katika inchi ya kigeni?

5Ee Yerusalema, kama nikikusahau,

mukono wangu wa kuume ukauke!

6Ulimi wangu ukuwe muzito,

kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalema,

nisipokufurahia kuliko furaha yangu kubwa!

7Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda,

siku ile Yerusalema iliponyanganywa;

kumbuka maneno haya waliyosema:

“Mubomoe Yerusalema!

Muongoe hata na misingi yake!”

8Ee Babeli, muharibifu wee!

Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutendea!

9Heri yule atakayetwaa watoto wako

na kuwapondaponda juu ya jiwe!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help