1kandokando ya mito ya Babeli tuliikaa tukilia,
tulipokumbuka Sayuni.
2Katika miti ya inchi ile,
tulitundika zeze zetu.
3Waliotupeleka kuwa watumwa walitaka tuwaimbie;
watesaji wetu walitaka tuwafurahishe, wakituambia:
“Mutuimbie nyimbo zimoja za Sayuni!”
4Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa Yawe
katika inchi ya kigeni?
5Ee Yerusalema, kama nikikusahau,
mukono wangu wa kuume ukauke!
6Ulimi wangu ukuwe muzito,
kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalema,
nisipokufurahia kuliko furaha yangu kubwa!
7Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda,
siku ile Yerusalema iliponyanganywa;
kumbuka maneno haya waliyosema:
“Mubomoe Yerusalema!
Muongoe hata na misingi yake!”
8Ee Babeli, muharibifu wee!
Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutendea!
9Heri yule atakayetwaa watoto wako
na kuwapondaponda juu ya jiwe!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.