Waroma 14 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Usimuhukumu ndugu yako

1Mumupokee yule anayekuwa zaifu katika imani pasipo kubishana naye juu ya mawazo yake.

2Kwa mufano, mutu mumoja kutokana na imani yake anaona kwamba anaweza kula kila chakula, lakini mwingine kutokana na imani yake zaifu, anakula tu mboga za majani.

3Yule anayekula kila chakula asimuzarau yule asiyekula kila chakula. Vilevile yule asiyekula kila chakula asimuhukumu yule anayekikula, kwa maana Mungu amemupokea.

4Wewe ni nani unayehukumu mutumishi wa mwingine? Akisimama imara katika kazi yake au akianguka, hilo ni shauri la bwana wake. Naye atasimama imara maana Bwana yuko na uwezo wa kumusimamisha.

5Watu wamoja wanahesabu siku fulani kuwa yenye maana zaidi kuliko siku zingine, lakini wengine wanahesabu siku zote kuwa sawasawa. Kwa hiyo kila mutu asadiki sawa vile anavyowaza yeye mwenyewe.

6Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.

7Kwa maana hakuna hata mutu mumoja kati yetu anayeishi kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe.

8Maana kama tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Bwana, na kama tunakufa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi ikiwa tunaishi, au ikiwa tunakufa, sisi ni watu wa Bwana.

9Ni kwa sababu hii Kristo alikufa na kufufuka kusudi apate kuwa Bwana wa waliokufa na wa wanaokuwa wazima vilevile.

10Lakini wewe, kwa sababu gani unamuhukumu ndugu yako? Au wewe kwa sababu gani unamuzarau ndugu yako? Maana sisi wote tutasimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Mungu.

11Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu:

“Bwana anasema:

Kama vile ninavyoishi, kila mutu atapiga magoti mbele yangu, na kila mutu ataitikia kwamba mimi ni Mungu.”

12Kwa hiyo kila mumoja kati yetu atajitetea mwenyewe kwa Mungu.

Usimukoseshe ndugu yako

13Basi tusihukumiane tena sisi wenyewe. Lakini tafazali mukamate kusudi hili: mutu asifanye kitu kinachoweza kumukwaza au kumwangusha ndugu yake katika zambi.

14Kufuatana na vile ninaungana na Bwana Yesu, ninajua hakika kwamba hakuna kitu kinachohesabiwa kichafu katika hali yake ya asili. Lakini kama mutu akihesabu kwamba kitu fulani ni kichafu, basi kitu kile ni kichafu kwake.

15Kama ukimuhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, wewe hautendi tena kufuatana na upendo. Kwa njia ya chakula chako usimupoteze mutu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.

16Basi musikubali kitu kile kinachoonekana kwenu kuwa kizuri kizarauliwe.

17Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu.

18Na yeyote anayemutumikia Kristo kwa njia hiyo anamupendeza Mungu, naye anapata kuwa mwenye kustahili mbele ya watu.

19Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.

20Usiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya maneno ya chakula. Hakika vyakula vyote vinaruhusiwa kukuliwa, lakini ni vibaya kwa mutu kula chakula kinachoweza kukwaza mwingine.

21Ni vema kuacha kula nyama, kunywa divai na kujizuiza kufanya chochote kinachoweza kumukwaza ndugu yako.

22Ulinde kwa ajili yako mwenyewe kile unachoaminia juu ya mambo yale mbele ya Mungu. Heri mutu asiyejihukumu katika kusudi lake.

23Lakini mutu anayekuwa na mashaka juu ya chakula anachokula, Mungu anamuhukumu, kwa sababu hatendi kufuatana na imani. Na kitendo chochote kisichotokana na imani ni zambi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help