1“Hii ndiyo amri, masharti na maagizo ambayo Yawe, Mungu wenu, aliniamuru niwafundishe, kusudi muyatimize katika inchi munayokwenda kuirizi.
2Wakati wote munapokuwa wazima, mutapaswa kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kutii masharti yote na amri ninazowapa ninyi na wazao wenu kusudi mupate kuishi maisha marefu.
3Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.
4“Basi musikilize, enyi Waisraeli! Yawe, Yawe tu, ni Mungu wetu.
5Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.
6Muweke ndani ya moyo wenu maneno hayo ninayowaamuru leo
7na kuwafundisha kwa uangalifu watoto wenu. Mutawaelezea mutakapokuwa munakaa katika nyumba au munapokuwa katika safari au munapolala au munapoamuka.
8Muyafunge katika mikono yenu na kuyavaa katika paji za nyuso zenu kama vile ukumbusho.
9Muyaandike kwenye miimo ya milango yenu na milango ya miji yenu.
Onyo kwa watu wasiotii10“Kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, yeye atawapa inchi yenye miji mikubwa na mizuri iliyostawi ambayo ninyi hamukuijenga.
11Nyumba zitakuwa zimejaa vitu vizuri ambavyo ninyi hamukuviweka, kutakuwa visima ambavyo hamukuchimba na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamukuyapanda. Yawe atakapowapeleka kwenye inchi hiyo ambako mutakuwa na chakula chote munachohitaji,
12muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.
13Mutamwogopa Yawe, Mungu wenu, mutamutumikia yeye peke yake na kuapa katika jina lake peke yake.
14Musiabudu miungu mingine, miungu ya watu wanaokuwa jirani nanyi,
15hasira ya Yawe isiwake juu yenu, naye asiwafute katika dunia, maana Yawe, Mungu wenu, anayekuwa kati yenu, ni Mungu mwenye wivu.
16“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.
17Muhakikishe kwamba munatii amri, maagizo, na masharti ya Yawe, Mungu wenu, ambayo amewaamuru.
18Mufanye yale yanayomupendeza Yawe, kusudi mupate kufanikiwa. Mutaweza kuirizi inchi ile nzuri ambayo Yawe aliapa kuwapa babu zenu,
19na mutawafukuza waadui zenu kama vile Yawe alivyoahidi.
20“Siku zinazokuja, mwana wako atakapokuuliza: ‘Maana ya maagizo, masharti na maamuzi ambayo Yawe, Mungu wetu, aliwaamuru kutenda ni nini?’
21Ninyi mutawajibu hivi: ‘Sisi tulikuwa watumwa wa mufalme wa Misri, na Yawe akatuokoa kwa mukono wake wenye nguvu.
22Kwa macho yetu wenyewe tulimwona akifanya vitambulisho na miujiza na mambo ya kutisha na ya ajabu juu ya Wamisri, mufalme wao na wakubwa wake.
23Alitutoa Misri, akatuleta hapa na kutupa inchi hii, kama vile alivyoapa kwamba atawapa babu zetu.
24Basi, Yawe akatuamuru kutii masharti haya yote na kumwogopa kwa faida yetu wenyewe, apate kutulinda siku zote kama hivi leo.
25Tukiwa waangalifu tukitimiza amri zote mbele ya Yawe, Mungu wetu, kama vile alivyotuamuru, tutahesabiwa kuwa wenye haki’.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.