Maombolezo UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu hiki kidogo cha Maombolezo ni mukusanyiko wa mashairi tano, ambamo mwandishi anaomboleza juu ya kuteketezwa kwa Yerusalema mwaka 586 mbele ya Kristo. Katika ibada za Wayuda mashairi hayo yalitumiwa kila mwaka kwa wakati wa kukumbuka kuharibiwa kwa hekalu la kwanza.Mashairi ine ya kwanza katika Kiebrania yameandikwa kwa kufuata utaratibu wa alfabeti 22 za Kiebrania. Kutokana na matengeneo hayo, sura 1, 2 na 4 zina aya 22, wakati sura ya 3 ina aya 66.