Matayo 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufano wa karamu ya ndoa(Lk 14.15-24)

1Yesu akaendelea kusema na lile kundi la watu kwa mifano. Akawaambia:

2“Ufalme wa mbinguni unafanana na mufalme mumoja aliyemufanyia mwana wake karamu ya ndoa.

3Yeye akawatuma watumishi wake kwa kuwaita watu wale walioalikwa kwa karamu, lakini hawakutaka kufika.

4Kisha akawatuma watumishi wengine, akisema: ‘Mwende kuwaambia waalikwa kwamba karamu yangu iko sasa tayari. Nimechinja ngombe na nyama wenye kunona; vitu vyote viko tayari. Muwaambie wafike kwa karamu!’

5Lakini wale waalikwa hawakushugulika na aliko lake; wakajiendea: mumoja kwenye shamba lake, mwingine kwenye biashara yake,

6na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatesa na kuwaua.

7Halafu mufalme akakasirika. Akawatuma waaskari wake kuwaua wale wauaji na kuteketeza muji wao kwa moto.

8Kisha akawaambia watumishi wake: ‘Karamu ya ndoa iko tayari, lakini si wale walioalikwa ndio waliostahili kuikula.

9Basi muende kwenye masanganjia, na watu wote mutakaowaona, muwaalike wafike kwa karamu.’

10Nao watumishi wakaenda katika barabara, wakakusanya watu wote waliowaona, wabaya na wazuri, na nyumba ya karamu ikajaa na wageni.

11“Naye mufalme alipoingia kwa kuwaangalia wale wageni, akamwona mutu mumoja asiyevaa nguo ya karamu.

12Akamwuliza: ‘Rafiki, namna gani umeingia hapa bila kuvaa nguo ya karamu?’ Lakini yule mutu hakumujibu neno.

13Halafu mufalme akawaambia watumishi wake: ‘Mumufunge mutu huyu miguu na mikono na kumutupa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’ ”

14Kisha, Yesu akasema: “Watu wanaoitwa ni wengi, lakini wale wanaochaguliwa ni wachache.”

Ulizo juu ya kulipakodi(Mk 12.13-17; Lk 20.20-26)

15Wafarisayo walienda kufanya shauri kusudi wapate kumunasa Yesu katika masemi.

16Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya:

“Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.

17Basi utuambie unafikiri nini: Sheria yetu inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana?”

18Lakini kwa kuwa Yesu alijua makusudi yao mabaya, akawajibu: “Ninyi wanafiki, kwa sababu gani munanipima?

19Munionyeshe feza inayotolewa kwa kulipa kodi.”

Basi wakamuletea kikoroti kimoja cha feza.

20Yesu akawauliza: “Sura hii na jina hili linaloandikwa hapa ni vya nani?”

21Wakamujibu: “Ni vya Mufalme wa Roma.”

Halafu Yesu akawaambia: “Basi mumupe Mufalme wa Roma vinavyokuwa vyake, na Mungu vinavyokuwa vyake.”

22Nao waliposikia jibu hili, wakashangaa sana, wakamwacha Yesu na kujiendea.

Ulizo juu ya ufufuko(Mk 12.18-27; Lk 20.27-40)

23Siku ile ile, Wasadukayo wamoja wakamufikia Yesu. (Watu hawa ndio wanaosema kwamba wafu hawatafufuka.)

24Wakamwuliza: “Mwalimu, Musa alisema: ‘Mutu akikufa bila kuacha mutoto, ndugu yake anapaswa kumwoa yule mujane na kumuzalia marehemu watoto.’

25Basi huku kwetu kulikuwa wandugu saba. Wa kwanza alioa mwanamuke, kisha akakufa bila kuzaa mutoto. Naye akamwachia ndugu yake yule mwanamuke.

26Na ikakuwa vile kwa ndugu wa pili na wa tatu na mpaka yule wa saba.

27Nyuma ya kufa kwa wote saba, yule mwanamuke akakufa vilevile.

28Sasa, siku wafu watakapofufuka, muke yule atakuwa wa nani, kwa maana wote saba walikuwa wamemwoa?”

29Yesu akawajibu: “Munadanganyika, kwa sababu ya kutojua Maandiko Matakatifu wala uwezo wa Mungu.

30Kwa maana wakati wafu watakapofufuka wataishi kama vile wamalaika wanavyoishi katika mbingu; hawataoa wala kuolewa.

31Na juu ya kufufuka kwa wafu, hamujasoma bado maneno haya Mungu aliyowaambia?

32‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ ” Yesu akaendelea kuwaambia: “Mungu si Mungu wa waliokufa, lakini ni Mungu wa wanaokuwa wazima.”

33Makundi ya watu waliposikia maneno hayo, wakashangaa sana na mafundisho yake.

Amri kubwa(Mk 12.28-34; Lk 10.25-28)

34Wafarisayo waliposikia kwamba Yesu aliwafungisha Wasadukayo kinywa, wakakusanyika pamoja.

35Na mumoja wao, aliyekuwa mwalimu mukubwa wa Sheria, akamufikia Yesu na kumwuliza hivi kwa kumupima:

36“Mwalimu, katika Sheria, ni amri gani inayokuwa kubwa katikati ya zote?”

37Yesu akamujibu: “ ‘Umupende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote.’

38Hii ndiyo amri inayokuwa kubwa zaidi, na ya kwanza.

39Na ya pili inayofanana nayo ni hii: ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’

40Amri hizi mbili ndicho kifungo cha Sheria yote ya Musa na mafundisho ya manabii.”

Ukoo wa ukubwa wa Kristo(Mk 12.35-37; Lk 20.41-44)

41Kwa kuona vile Wafarisayo walivyokuwa wamekusanyika, Yesu akawauliza:

42“Munafikiri nini juu ya Kristo? Yeye ni mwana wa nani?”

Nao wakamujibu: “Yeye ni mwana wa Daudi.”

43Na Yesu akawaambia: “Basi namna gani Daudi, akiongozwa na Roho, aliweza kumwita ‘Bwana’, akisema:

44‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu:

Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu

mpaka nitakapoweka waadui zako chini ya miguu yako.’

45“Basi ikiwa Daudi anamwita Kristo ‘Bwana,’ namna gani Kristo anaweza kuwa mwana wake?”

46Basi hakuna mutu aliyeweza kumujibu neno, na tangia siku ile hakuna aliyesubutu kumwuliza tena neno.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help