Zaburi 30 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maombi ya shukrani

1Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.

2Ninakutukuza,

ee Yawe,

maana umeniokoa,

wala haukuwaacha waadui zangu wanisimange.

3Ee Yawe, Mungu wangu,

nilikulilia, nawe ukaniponyesha.

4Ee Yawe, umeniokoa kutoka kuzimu;

umenipa tena uzima,

umenitoa kutoka kati ya wafu.

5Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake;

mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.

6Hasira yake inadumu muda kidogo tu,

upendo wake unadumu milele.

Kilio kinaweza kuwa usiku,

lakini muchana kunatokea furaha.

7Mimi nilipofanikiwa, nilisema:

“Sitashindwa hata kidogo!

8Kwa upendo wako, ee Yawe,

umeniimarisha kama mulima mukubwa.”

Lakini ukajificha mbali nami,

nami nikafazaika.

9Nilikulilia wewe, ee Yawe;

nilikusihi, ee Yawe:

10“Utapata faida gani nikikufa

na kushuka mpaka katika shimo la wafu?

Mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu?

Yanaweza kusimulia uaminifu wako?

11Usikie, ee Yawe, unihurumie;

ee Yawe, unisaidie!”

12Wewe umegeuza malalamiko yangu kuwa ngoma ya furaha;

umeniondolea huzuni yangu, ukanijaza furaha.

13Mimi nitakusifu wala sitakaa kimya.

Ee Yawe, Mungu wangu, nitakushukuru milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help