1Ole kwako Yerusalema, mazabahu ya Mungu,
muji ambamo Daudi alipiga kambi yake!
Miaka inakuja na kupita,
na sikukuu zako zinaendelea kufanyika;
2lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema,
ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo,
muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.
3Mimi nitapanga kundi la waaskari juu ya Yerusalema,
nami nitauzunguka na kuushambulia.
4Utaangushwa mbali sana ndani ya udongo,
kutoka kule mbali utatoa sauti,
maneno yako yatatoka kule chini katika mavumbi,
sauti yako itatoka ndani ya udongo kama ya muzimu.
5Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini,
waliokutendea ukali watakuwa kama maganda.
Hayo yatafanyika kwa rafla.
6Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia;
atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa;
atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.
7Halafu, kundi la mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema,
wote wanaoshambulia ukuta wake na kuutia wasiwasi,
watatoweka kama ndoto, kama maono ya usiku.
8Mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema
yatakuwa kama mutu mwenye njaa anayeota ndoto kwamba anakula
lakini anaamuka angali bado na njaa,
na kama mutu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa
lakini anaamuka muzaifu, na angali bado na kiu.
Hatari ya kuzarau maonyo9Mukuwe wapumbafu na kupumbazika:
mupofuke na kuwa vipofu!
Mulewe lakini si kwa divai;
mupepesuke lakini si kwa pombe.
10Yawe amewamwangia roho ya usingizi;
macho yenu yasipate kuona enyi manabii,
amefunika vichwa vyenu enyi wenye kupata maono.
11Basi, kwenu ninyi, maono haya yote ni kama ujumbe ulioandikwa katika kitabu kilichofungwa kwa muhuri. Ukimupelekea mutu yeyote anayejua kusoma, na kumwambia “Unisomee kitabu hiki”, atasema “Siwezi kukisoma kwa sababu kimefungwa kwa muhuri.”
Sayuni, jiwe la musingi12Na ukimupa mutu yeyote asiyejua kusoma, na kumwambia “Unisomee kitabu hiki”, atasema: “Sijui kusoma.”
13Bwana anasema:
Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu,
lakini mioyo yao iko mbali nami.
Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu,
jambo walilojifunza wao wenyewe.
14Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu,
mambo ya ajabu na ya kushangaza.
Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima,
na akili ya wenye akili wao itatoweka. Tumaini siku zinazokuja.
15Ole kwenu ninyi munaomuficha Yawe mipango yenu,
munaotenda matendo yenu katika giza
na kusema: Hakuna atakayetuona;
nani anayeweza kujua tunachofanya?
16Ninyi munafanya mambo kinyume kabisa!
Mufinyanzi na udongo ni hali moja?
Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza hivi:
Wewe haukunitengeneza.
Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba;
Wewe haujui kitu.
17Bado kidogo tu,
pori la Lebanoni litageuzwa kuwa shamba lenye udongo muzuri,
na shamba lenye udongo muzuri kuwa pori.
18Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa katika kitabu
na kutoka katika giza, vipofu wataanza kuona.
19Wanyenyekevu watapata furaha mupya kwa Yawe,
na wamasikini kati ya watu watashangilia kwa furaha,
kwa sababu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.
20Watesaji watatoweka,
wenye kumuchekelea Mungu watakwisha,
wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.
21Watatoweka wale wanaopotosha maneno ya mutu katika tribinali,
watu wanaowatega waamuzi
na wanaosema uongo kwa kuwanyima haki yao wasiokuwa na kosa.
22Kwa hiyo, Yawe aliyemukomboa Abrahamu,
anasema hivi juu ya wazao wa Yakobo:
Wazao wa Yakobo hawatapata haya tena,
hawatainamisha vichwa vyao tena kwa ajili ya haya.
23Watakapowaona watoto wao,
watoto niliowajalia mimi mwenyewe,
watalitukuza jina langu mimi Mutakatifu wa Yakobo,
watakuwa na heshima kwangu mimi Mungu wa Israeli.
24Waliopotoka katika roho watapata maarifa
na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.