Hesabu 29 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Sadaka ya sikukuu ya mwaka mupya(Law 23.23-25)

1Siku ya kwanza ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi. Hiyo ni siku ya kupiga baragumu.

2Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe wasiokuwa na kilema chochote.

3Mutatoa vilevile sadaka yake ya vyakula ya unga safi uliochanganywa na mafuta: kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume,

4na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

5Tena mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.

6Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya mwezi mupya na sadaka yake ya vyakula, na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji kama vile inavyoagizwa. Itakuwa harufu nzuri yenye kupendeza; ni sadaka kwa Yawe iliyoteketezwa kwa moto.

Matoleo ya siku ya kufanyiwa musamaha(Law 23.26-32)

7Siku ya kumi ya mwezi wa saba mutafanya mukutano mutakatifu. Siku hiyo munapaswa kufunga kula na musifanye kazi. Ang. Law 16.29-34

8Mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu ya kumupendeza Yawe: mwana-ngombe mumoja, kondoo dume mumoja, wana-kondoo saba wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.

9Zaidi ya vitu hivi mutatoa sadaka ya unga safi uliochanganywa na mafuta kilo tatu pamoja na huyo ngombe dume, kilo mbili pamoja na yule kondoo dume,

10na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

11Mutatoa vilevile beberu mumoja kwa sadaka kwa ajili ya zambi zaidi ya sadaka ya kufanyiwa upatanisho, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji.

Sadaka ya sikukuu ya vibanda(Law 23.33-43; Kumb 16.13-17)

12Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Hamutafanya kazi siku hiyo. Mutafanya sikukuu kwa ajili ya Yawe kwa siku saba.

13Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, yenye harufu nzuri inayomupendeza Yawe: wana-ngombe dume kumi na watatu, kondoo dume wawili, wana-kondoo kumi na wane wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.

14Sadaka itakayoandamana nazo itakuwa unga safi uliochanganywa na mafuta: kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo,

15na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

16Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

17Siku ya pili mutatoa: wana-ngombe dume kumi na wawili, kondoo dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wane, wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

18Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za vinywaji pamoja na wale wana-ngombe dume, kondoo na wana-kondoo, kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

19Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

20Siku ya tatu mutatoa: ngombe dume kumi na mumoja, kondoo wawili, wana-kondoo kumi na wane wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.

21Mutawatolea pamoja na sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

22Vilevile mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

23Siku ya ine mutatoa: ngombe dume kumi, kondoo dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wane, wasiokuwa na kilema.

24Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume na kondoo na wana-kondoo kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

25Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

26Siku ya tano, mutatoa ngombe dume tisa, kondoo wawili, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

27Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume na kondoo na wana-kondoo kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

28Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

29Siku ya sita mutatoa ngombe dume wanane, kondoo dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

30Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume, kondoo dume na wana-kondoo kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

31Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji.

32Siku ya saba mutatoa ngombe dume saba, kondoo dume watatu, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.

33Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume, kondoo dume, na wana-kondoo, kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

34Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

35Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu. Musifanye kazi siku hiyo.

36Mutatoa sadaka ya kuteketezwa yenye harufu nzuri inayomupendeza Yawe: ngombe dume mumoja, kondoo dume mumoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

37Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na huyo ngombe dume, huyo kondoo dume, na wale wana-kondoo kulingana na hesabu yao kama vile inavyoagizwa.

38Vilevile mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka ya kinywaji.

39Haya ndiyo maagizo juu ya sadaka mutakazomutolea Yawe wakati wa sikukuu zenu zilizopangwa. Zaidi ya hizi zote, kuna vilevile sadaka za kuteketezwa, za vyakula na za kinywaji, za kutimiza kiapo na za mapenzi, na za amani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help