1Basi, Musa akiwa pamoja na wazee wa Israeli aliwaambia watu hivi: “Mushike amri zote ninazowapa leo.
2Siku ile mutakapovuka muto Yordani na kuingia katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa, mutasimika mawe makubwa na kuyapiga lipu.
3Juu yake mutaandika maneno yote ya sheria hizi zote, mutakapoingia katika inchi ile inayotiririka maziwa na asali, ambayo Yawe, Mungu wa wazee wenu, aliwaahidi.
4Mukiwa ngambo ya muto Yordani, mutasimika mawe hata juu ya mulima Ebali, kama vile ninavyowaamuru hivi leo, na kuyapiga lipu.
5Mutamujengea Yawe, Mungu wenu, mazabahu pahali pale panapokuwa na mawe ambayo hayakuchongwa.
6Mutamujengea Yawe, Mungu wenu, mazabahu kwa mawe yasiyochongwa. Juu ya mazabahu hiyo mutamutolea Yawe, Mungu wenu, sadaka za kuteketezwa.
7Mutamutolea sadaka za amani, na kula hapohapo na kufurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu.
8Mutaandika waziwazi juu ya mawe hayo maneno yote ya sheria hii.”
9Basi, Musa pamoja na makuhani Walawi wakawaambia watu wote wa Israeli: “Munyamaze munisikilize enyi watu wa Israeli. Leo hii ninyi mumekuwa watu wa Yawe, Mungu wenu.
10Kwa hiyo mutatii sauti ya Yawe, Mungu wenu, mukifuata amri zake na masharti yake ambayo ninawaamuru leo.”
Laana ya kutokutii11Siku hiyo Musa akawaagiza watu na kusema:
12“Mukisha kuvuka Yordani, makabila haya yatasimama juu na mulima Gerizimu kwa kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benjamina.
13Na makabila haya yatasimama juu ya mulima Ebali wakati laana zitakapotolewa: Rubeni, Gadi, Aseri, Zebuluni, Dani na Nafutali.
14Nao Walawi watatangazia watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
16“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayezarau baba yake au mama yake.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
17“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeondoa kitambulisho cha mupaka wa mwenzake.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
18“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayemupotosha kipofu katika njia.’ Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
19“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
20“ ‘Alaaniwe mwanaume anayelala na muke wa baba yake, maana amemupatisha baba yake haya’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
21“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayelala na nyama yoyote’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
22“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayelala na dada yake akuwe ni binti ya baba yake au binti ya mama yake’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
23“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayelala na mama mukwe wake’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
24“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeua mutu kwa siri’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
25“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepokea kituliro kusudi aue mutu asiyekuwa na kosa’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
26“ ‘Alaaniwe mutu yeyote asiyekubali maneno haya ya sheria na kuyatii’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.