1Maneno ya mufalme Lemueli. Mashauri aliyopewa na mama yake:
2Nikuambie nini mwana wangu?
Nikuambie nini mwana wangu niliyezaa?
Nikuambie nini wewe niliyeomba kwa Mungu?
3Usimalize nguvu zako kwa wanawake,
usiwape mali yako wale wanaoangamiza wafalme.
4Haifai, ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai,
wala wakubwa kutamani vileo.
5Wakikunywa watasahau maagizo ya sheria,
na kuwanyima haki wenye taabu.
6Umupe mutu anayekaribia kufa kinywaji kikali,
uwape divai wale wenye huzuni tele;
7wakunywe na kusahau umasikini wao,
wasikumbuke tena taabu yao.
8Lakini wewe, useme kwa ajili ya wote wanaokuwa bubu;
na kutetea haki za wote wasiojiweza.
9Sema kwa ajili yao na kuamua kwa haki,
linda haki za wamasikini na wakosefu.
Muke mwema10Muke mwema atapatikana wapi?
Bei yake ni kali kuliko ushanga!
11Mume wake anamwamini kwa moyo
na hatakosa faida.
12Hamutendei mume wake mabaya hata kidogo,
lakini anamutendea mazuri maisha yake yote.
13Anatafuta sufu na kitani,
na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.
14Yeye ni kama mashua za biashara:
analeta chakula chake kutoka mbali.
15Anaamuka mbele ya mapambazuko
kwa kutayarishia jamaa yake chakula
na kuwagawanyia kazi watumishi wake.
16Anafikiri kununua shamba, kisha analinunua,
na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.
17Yuko tayari kufanya kazi kwa nguvu
na kuimarisha mikono yake.
18Anatambua kwamba shuguli zake zina faida;
anafanya kazi hata usiku kwa mwangaza wa taa yake.
19Anasokota nyuzi kwa mikono yake mwenyewe,
kwa vidole vyake mwenyewe anasuka nguo zake.
20Anafungua mukono wake kwa kuwapa wamasikini,
ananyoosha mukono kwa kusaidia wakosefu.
21Haogopi juu ya jamaa lake wakati wa baridi kali,
maana kila mutu yuko na nguo za kutosha.
22Anajitengenezea matandiko,
nguo zake ni za rangi nyeusi-nyekundu za kitani safi.
23Mume wake ni mutu mwenye kuheshimiwa katika baraza,
anapoikaa katikati ya wazee wa inchi.
24Mwanamuke huyu anatengeneza nguo na kuziuzisha,
anawauzishia wachuuzi mikaba.
25Nguvu na heshima ndizo sifa zake.
Anacheka anapofikiri juu ya wakati unaokuja.
26Anafungua kinywa kwa kusema kwa hekima;
anawashauri wengine kwa wema.
27Anachunguza yote yanayofanyika katika nyumba yake;
hakai bure hata kidogo.
28Watoto wake wanaamuka na kumushukuru,
mume wake anaimba sifa zake.
29Anasema: “Wanawake wengi wametenda mambo ya ajabu,
lakini wewe umewashinda wote.”
30Mapendezi ni udanganyifu na uzuri wa uso haukawii,
lakini mwanamuke anayemwogopa Yawe atasifiwa.
31Jasho lake linastahili kulipwa.
Shuguli zake zinapaswa kuheshimiwa popote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.