1Zaburi ya Daudi. Inaelekea wakati alipomukimbia mwana wake Abusaloma.
2Ee Yawe,
angalia ginsi waadui zangu wanavyokuwa wengi.
Ni wengi sana hao wanaonishambulia.
3Wengi wanasema juu yangu:
“Hautapata musaada wowote kwa Mungu.”
4Lakini wewe, ee Yawe, unanizunguka kama ngao;
kwako ninapata utukufu na ushindi.
5Ninakulilia kwa sauti, ee Mungu,
nawe unanisikiliza kutoka kwenye mulima wako mutakatifu.
6Ninalala na kupata usingizi,
ninaamuka tena, maana wewe ni tegemeo langu.
7Sitaogopa maelfu ya watu
wanaonizunguka kila upande.
8Ee Yawe,
ee Mungu wangu,
wewe unayevunja waadui zangu wote mataya,
unayeponda waovu meno,
simama sasa uniokoe!
9Yawe ndiwe unayeokoa;
uwape baraka watu wako.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.