Zaburi 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuomba musaadaFuraha ya kweli

1Zaburi ya Daudi. Inaelekea wakati alipomukimbia mwana wake Abusaloma.

2Ee Yawe,

angalia ginsi waadui zangu wanavyokuwa wengi.

Ni wengi sana hao wanaonishambulia.

3Wengi wanasema juu yangu:

“Hautapata musaada wowote kwa Mungu.”

4Lakini wewe, ee Yawe, unanizunguka kama ngao;

kwako ninapata utukufu na ushindi.

5Ninakulilia kwa sauti, ee Mungu,

nawe unanisikiliza kutoka kwenye mulima wako mutakatifu.

6Ninalala na kupata usingizi,

ninaamuka tena, maana wewe ni tegemeo langu.

7Sitaogopa maelfu ya watu

wanaonizunguka kila upande.

8Ee Yawe,

ee Mungu wangu,

wewe unayevunja waadui zangu wote mataya,

unayeponda waovu meno,

simama sasa uniokoe!

9Yawe ndiwe unayeokoa;

uwape baraka watu wako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help