1Musikilize, enyi watu wa Yakobo,
enyi munaojulikana kwa jina la Israeli,
ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda.
Ninyi munaapa kwa jina la Yawe,
na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli;
lakini hayo si ukweli wala sawa.
2Ninyi munaona utukufu kujiita watu wa muji mutakatifu,
na kujidai kumutegemea Mungu wa Israeli,
ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi.
3Nilitangaza zamani matukio ya mbele,
niliyatangaza mimi mwenyewe
na kuyafanya yajulikane kwenu.
Mara moja nikaanza kuyatimiza,
nayo yakapata kutukia.
4Lakini nilikujua wewe kuwa na moyo mugumu;
kichwa kigumu kama chuma,
uso wako kama shaba.
5Kwa hiyo nilikutangazia mambo yale tangu zamani,
mbele hayajatukia, mimi nilikujulisha,
kusudi usiseme: Ni sanamu yangu iliyotenda mambo hayo,
sanamu zangu za chuma ndizo ziliyaagiza.
6Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote.
Kwa nini hauwezi kuyakubali?
Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya;
mambo yaliyofichwa ambayo haukuyajua.
7Mambo hayo yanatukia sasa;
haukupata kuyasikia mbele ya siku ya leo,
hivyo hauwezi kusema: Aa! Nilikwisha kuyajua.
8Haujapata kuyasikia wala kuyajua hata kidogo;
tangu zamani masikio yako hayakuyasikia.
Nilijua kwamba wewe ni mudanganyifu,
na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.
9Kwa heshima ya jina langu,
ninatuliza hasira yangu;
kwa ajili ya heshima yangu,
ninajizuiza kusudi nisikuangamize.
10Mimi nimekusafisha lakini si kama feza katika furu.
Nimewapima katika furu ya taabu.
11Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe.
Kwa nini jina langu lizarauliwe?
Siwezi kumupatia mwingine utukufu wangu!
Kiro, muchaguliwa wa Yawe12Unisikilize ee taifa la Yakobo,
unisikilize ee Israeli niliyekuita.
Mimi ndiye.
Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
13Kwa mukono wangu niliuweka musingi wa dunia,
mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu.
Nikiziita mbingu na dunia,
zinasimama haraka mbele yangu.
14Mukusanyike wote musikilize!
Nani kati yenu alitabiri vitu hivi?
Yule ambaye Yawe anamupenda
atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli,
atawashambulia Wakaldea.
15Mimi –ni mimi!– nimesema na kumwita;
nimemuleta, naye atafanikiwa katika mupango wake.
16Musogee karibu nami musikie jambo hili:
Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri,
tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwa pale.
Sasa, Bwana wetu Yawe amenituma,
na kunipa nguvu ya Roho wake.Mupango wa Mungu kwa watu wake
17Yawe, Mutakatifu wa Israeli,
Mukombozi wako, anasema hivi:
Mimi ndiye Yawe, Mungu wako;
ninayekufundisha kwa faida yako
na kukuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.
18Ingekuwa heri ungalizitii amri zangu!
Halafu baraka zingekutiririkia kama muto,
ungefanikiwa kwa wingi kama mawimbi ya bahari.
19Wazao wako wangekuwa wengi
kama muchanga,
kama chembe za muchanga.
Jina lao lisingalisahauliwa hata kidogo,
wala halingalifutwa mbele yangu.
20Sasa, muondoke Babeli!
Mukimbie kutoka kwa Wakaldea!
Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe.
Mueneze habari zake kila pahali katika dunia.
Museme: Yawe amekomboa
taifa la mutumishi wake Yakobo.
21Alipowaongoza katika jangwa hawakuona kiu,
aliwatiririshia maji kutoka katika jiwe,
alipasua jiwe maji yakabubujika.
22Lakini Yawe anasema hivi:
Hakuna amani kwa watu waovu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.